RAIS wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan amemteua aliyekuwa mwandishi na mtangazaji wa Shirika la Utangazaji la Uingereza (BBC), Zunura Yunus kuwa Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais Ikulu. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).
Zuhura ambaye ni Mtanzania anachukua nafasi ya Jaffar Haniu ambaye atapangiwa kazi nyingine.
Zuhura ambaye ameitumikia BBC kwa miaka 14, hivi karibuni alitangaza kuachia ngazi ndani ya shirika hilo kubwa duniani.
Taarifa ya Kaimu Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais Ikulu, Jaffar Haniu aliyoitoa leo Jumanne, tarehe 1 Februari 2022 imeeleza uteuzi huo umeanza 30 Januari 2022.
Leave a comment