Thursday , 2 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Rais Samia amlilia Jecha Salim Jecha
Habari za Siasa

Rais Samia amlilia Jecha Salim Jecha

Spread the love

RAIS Samia Suluhu Hassan ametuma salamu za rambirambi kutokana na kifo cha aliyewahi kuwa Mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi Zanzibar (ZEC), Jecha Salim Jecha. Anaripoti Mwandishi Wetu …(endelea).

Jecha ambaye aliyekuwa Mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi Zanzibar (ZEC) kuanzia tarehe 30 Aprili 2013 hadi tarehe 29 Aprili 2018, amefariki dunia leo Jumanne katika Hospitali ya Jeshi Lugalo jijini Dar es Salaam.

Aidha, kupitia taarifa kwa vyombo vya habari iliyotiwa saini na Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais Ikulu, Zuhura Yunus, Rais Samia imesema;

“Rais Samia amepokea taarifa za kifo cha marehemu Jecha kwa majonzi makubwa na masikitiko makubwa,” imeeleza sehemu ya taarifa hiyo.

Mbali na salamu kuhusu msiba wa Jecha, Rais Samia pia ametuma salamu za rambirambi kwa familia ya Rais wa awamu ya tatu, Hayati Benjamin Mkapa, kutokana na kifo cha Bernard Mkapa (kaka wa Hayati Benjamin Mkapa).

“Rais Samia amewaomba wanafamilia wote wawe na moyo wa uvumilivu katika kipindi hiki kigumu cha majonzi na anawaombea marehemu wote wapumzike mahali pema peponi, Amina,” imeeleza taarifa hiyo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaKimataifa

Mwanamke Rwanda ataka kupambana tena na Kagame

Spread the loveKIONGOZI wa kihistoria wa upinzani nchini Rwanda, Victoire Ingabire Umuhoza,...

Habari za Siasa

Wizara ya Kilimo yapanga kutumia Sh. 1.2 trilioni 2024/25

Spread the loveWIZARA ya Kilimo, imepanga kutumia bajeti ya Sh. 1.2 trilioni...

Habari za SiasaTangulizi

Serikali yaanza msako wanaotoa mikopo kausha damu

Spread the loveSERIKALI imeanza kufuatilia watu, vikundi na taasisi zinazotoa kinyume cha...

Habari za Siasa

Spika Tulia aibana Serikali mafao ya wastaafu Jumuiya ya Afrika Mashariki

Spread the loveSPIKA wa Bunge, Dk. Tulia Ackson ameitaka Serikali kufanya tathimini...

error: Content is protected !!