Mahakama ya Mkoa wa Vuga mjini Unguja imemwachia huru mshtakiwa Ramadhan Ali maarufu kama Afande Rama aliyekuwa akikabiliwa na mashtaka ya kuingiliwa kinyume na maumbile. Anaripoti Mwandishi Wetu …(endelea).
Afande Rama ameachiwa huru leo Jumanne baada ya hakimu wa mahakama hiyo, Khamis Simai kudai kuwa mshtakiwa hana hatia chini ya kifungu cha 220 ya sheria namba 7 ya mwaka 2018.
Kesi hiyo namba 59 ya mwaka 2023 ilianza kusikilizwa mahakamani hapo ambapo jumla ya mashahidi tisa kutoka upande wa mwendesha mashtaka waliwasilisha ushahidi wao ambao hawakuweza kumtia hatiani mtuhumiwa.
Ramadhani alishtakiwa baada ya kusambaa kwa video katika mitandao ya kijamii zilizodhaniwa kuwa ni yeye ambaye alionekana akishiriki tendo la kuingiliwa kinyume na maumbile.
Upande wa mashtaka ulikuwa unawakilishwa na muendesha mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashtaka Zanzibar Mohd Saleh.
Afande Rama ambaye alikuwa Askari wa kikosi cha kutuliza gasia, kabla ya kushtakiwa, alivuliwa cheo cha uaskari na kubaki raia wa kawaida.
Leave a comment