Saturday , 11 May 2024
Home Habari Mchanganyiko Rais Samia afuta tozo 6% bodi ya mikopo
Habari Mchanganyiko

Rais Samia afuta tozo 6% bodi ya mikopo

Spread the love

 

RAIS wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan, amefuta tozo ya asilimia sita, inayotozwa kila mwaka na Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu (HESLB), kwa wanufaika wa mikopo hiyo, kwa ajili ya kutunza thamani ya fedha. Anaripoti Regina Mkonde, Dar es Salaam … (endelea).

Rais Samia amefuta tozo hiyo, leo Jumamosi tarehe 1 Mei 2021, akihutubia katika maadhimisho ya sherehe za wafanyakazi duniani ‘Mei Mosi’, zilizofanyika Uwanja wa CCM, jijini Mwanza.

Mbali na kufutwa kwa tozo hiyo, amesema makato ya asilimia 15 yanayokatwa kila mwezi kwenye mshahara wa mnufaika wa mikopo hiyo kila mwezi, itabaki kama ilivyo.

“Changamoto nyingine ni makato ya HELSB, kwenye changamoto hii tumeamua kubakia na asilimia 15 inayokatwa na Serikali imeamua kufuta asilimia sita tuliyokuwa tukikata zaidi,” amesema Rais Samia.

Kiongozi huyo wa Tanzania amefuta tozo hiyo, baada ya Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi Tanzania (TUCTA), kuiomba Serikali ipunguze mzigo wa makato kwa wanufaika wa mikopo hiyo.

Aidha, Rais Samia amewaagiza wanufaika wa mikopo ya HELSB, waendelee kulipa mikopo hiyo.

“Tusisitize kwamba, deni hili wale waliokopa waendelee kulipa na nichukue fursa hii kuwaagiza HELSB kuondoa asilimia 6,” ameagiza Rais Samia.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Vijana UVCCM Kagera wataka mwenyekiti wao ajiuzulu

Spread the loveVIJANA wa Chama cha Mapinduzi Mkoa wa Kagera wamemtaka Mwenyekiti...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

THRDC, Wizara ya Katiba wajadili uanzishaji haki binadamu katika biashara

Spread the loveMTANDAO wa Watetezi wa Haki za Binadamu Tanzania (THRDC), umefanya...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Sitta ang’ang’ana wanafunzi watibiwe bure, Serikali yagoma

Spread the loveMBUNGE wa Urambo, Margaret Sitta, ameishauri Serikali iweke utaratibu wanafunzi...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Waitara ahoji bungeni mwarobaini mauaji katika mgodi Barick North Mara

Spread the loveMBUNGE wa Tarime Vijijini (CCM), Mwita Waitara, ameitaka Serikali kutafuta...

error: Content is protected !!