Friday , 26 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Rais Samia aagiza darasa la saba, vyeti feki kulipwa mafao yao
Habari za Siasa

Rais Samia aagiza darasa la saba, vyeti feki kulipwa mafao yao

Rais wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan
Spread the love

 

RAIS wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan, ameagiza watumishi wa umma waliofukuzwa kazi kutokana na sababu mbalimbali ikiwemo vyeti vya kughushi ‘feki’, walipwe stahiki zao. Anaripoti Mwandishi Wetu, Mwanza … (endelea).

Rais Samia ameagiza hayo leo Jumamaosi, tarehe 1 Mei 2021, katika maadhimisho ya siku ya wafanyakazi duniani ‘Mei Mosi’, yaliyofanyika kitaifa, Uwanja wa CCM Kirumba, jijini Mwanza.

Rais Samia amewaagiza waajiri wote kufuata sheria kwa kuwalipa wafanyakazi hao stahiki zao.

“Natumia fursa hii kurudia maelezo ya serikali kwa waajiri kufuata sheria katika kuhitimisha ajira za watumishi walioajiriwa darasa la saba na kughushi vyeti na waliostaafishwa.”

“Wako waliolipwa na wako hawajalipwa kutokana na madai kwamba serikali bado haikutoa muongozo mahsusi wa kulipa mafao,” amesema Rais Samia.

Rais huyo wa Tanzania amesema “wapo hawajalipwa kwa kutokuwepo kwa kumbukumbu za ajira zao, niwaagize wajiri waliokuwa na wafanyakazi wa aina hii wafanye inavyowezekana kila mwenye haki apatiwe haki yake.”

Ameiagiza Wizara ya Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi na Utawala Bora, kusimamia suala hilo.

5 Comments

  • Tunaomba maagizo ya Rais nisheria ameagiza mei mosi 2021 likapuuzwa ameagiza mei mosi 2022 mpaka leo kimya hivi nikipi kinafanya huyu Rais maelekezo na maagizo yake yana puuzwa? Nikitugani kilikuwa kinawasukuma kutekeleza maagizo ya hayati Rais Magufuli hata kabla hashuka jukwaani? Hivi Rais ange agiza watumishi hao wakamatwe agizo hilo lingesubiri muongozo? Naamini siku hiyohiyo wangelikamatwa muongozo ungefuata baadae . Nimuombe mh Rais apaze sauti awaite Ikulu awasikilize mwenyewe shida waliyo Mayo watanzania hawa Wafungwa wanathamani kuliko watumishi hao waliolitumikia Taifa lao kwa uaminifu kosa kukosa cheti cha kidato cha 4 pamoja nakuwa kinachofanya kazi in taaluma siyo cheti cha kidato cha 4 kama cheti cha kidato cha 4 ndiyo taaluma tusingekuwa na upungufu WA watumishi tungekuwa tunawasambaza kila wanapo hitimu kidato cha 4 wanaingia kazini moja kwa moja

  • Tunamwomba rais awakumbushe watu wa utumishi watushughulikie maagizo yake kwani naona wanamdhalau.kila nikienda psspf naambiwa hakuna mwongozo.tuna hali mbaya sana natumitunikia taifa zaidi ya miaka 20.mara ya mwisho nimetoka jana.tr25.10.2022

  • Tunamshukuru Sana Rais wetu Mpendwa Mama yetu pamoja na Viongozi Wote kukubaliana na swala hili la kuturejeshea haki zetu na bila kuwasahau watumishi wa Mifuko ya Jamii
    watakaotumia muda wao kutuhudumia ,Hatuna chakuwalipa kitakacholingana na fadhila zenu Bali tunaesombea Maisha careful na Utumishi Mwema ,

  • Tunamshukuru Sana Rais wetu Mpendwa Mama yetu pamoja na Viongozi Wote kukubaliana na swala hili la kuturejeshea haki zetu na bila kuwasahau watumishi wa Mifuko ya Jamii
    watakaotumia muda wao kutuhudumia ,Hatuna chakuwalipa kitakacholingana na fadhila zenu Bali tunaesombea Maisha careful na Utumishi Mwema ,

  • Tunamshukuru Sana Rais wetu Mpendwa Mama yetu pamoja na Viongozi Wote kukubaliana na swala hili la kuturejeshea haki zetu na bila kuwasahau watumishi wa Mifuko ya Jamii
    watakaotumia muda wao kutuhudumia ,Hatuna chakuwalipa kitakacholingana na fadhila zenu Bali tunawaombea Maisha memal na Utumishi Mwema ,

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

Habari za SiasaTangulizi

Biteko ataja vipaumbele 7 bajeti nishati 2024/25

Spread the love  NAIBU Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mwekezaji amwaga bil. 39 kujenga viwanda 3 vya uchenjuaji

Spread the loveKampuni ya Mineral Access System Limited (MAST) inayoiwakilishwa kampuni ya...

error: Content is protected !!