Tuesday , 30 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Rais Faye amteua aliyekuwa mfungwa mwenzie kuwa waziri mkuu
Habari za SiasaKimataifa

Rais Faye amteua aliyekuwa mfungwa mwenzie kuwa waziri mkuu

Spread the love

Rais mpya wa Senegal, Bassirou Diomaye Faye, amemteua Ousmane Sonko kama Waziri Mkuu saa chache baada ya kuapishwa kuwa mkuu wa nchi hiyo jana Jumanne. Inaripoti Mitandao ya Kimataifa … (endelea).

Taarifa ya uteuzi huo ilisomwa jana jioni na Katibu Mkuu wa ofisi ya rais Senegal, Oumar Samba Bâ katika kituo cha televisheni ya taifa – RTS.

“Ninapima umuhimu wa imani ambayo Rais Faye ameniwekea,” amesema Ousmane Sonko kwenye RTS, wakati akimshukuru Faye na kumhakikishia uaminifu na kumuahidi kujitolea kwake katika ujenzi wa taifa hilo.

Sonko ambaye ni Mwanzilishi huyo wa chama cha PASTEF, licha ya kwamba hakuweza kuwa mgombea wa urais, ameweka historia ya kipekee kutokana na safari ya kisiasa ya wawili hao.

“Wakati wa mkutano ambao ulifunga kampeni zetu za uchaguzi, nilisema kwamba sote tunafanya kazi ya kumchagua Rais Bassirou Diomaye Faye. Hakutakuwa na suala la kumwacha peke yake kuchukua jukumu hili.

“Ningependa kuwaambia Wasenegali, kwa kila mmoja, popote pale alipo, kwamba jukumu hili ni lao. Kila mtu atalazimika kujitolea vilivyo zaidi ili tufikie malengo ambayo tumeweka kwa Senegal na sio kwa rais,” alisema Sonko.

Alisema serikali wanayoenda kuiunda watajitolea kwa hali na mali kuhakikisha wanayafikia malengo waliyowaahidi Wasenegali ambayo ni kuwakwamua katika mdororo wa uchumi,kuwaletea maendeleo na kuwa mfano wa mabadiliko ya kweli na sahihi.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Mavunde aomba bilioni 231.9 bajeti wizara ya madini

Spread the loveWAZIRI wa Madini, Anthony Mavunde leo Jumanne amewasilisha hotuba ya...

Habari za SiasaTangulizi

Lissu amjibu Fatma Karume kuhusu Rais Samia

Spread the love  MAKAMU Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema)...

Habari za SiasaTangulizi

Dk. Slaa: Watanzania iungeni mkono Chadema uchaguzi 2025

Spread the loveMWANASIASA mkongwe nchini Tanzania, Dk. Wilbroad Slaa, amewataka watanzania wakiunge...

Habari za SiasaTangulizi

Samia ataja miradi ambayo Tanzania inashirikiana na IDA

Spread the loveRais wa Tanzania Dk. Samia Suluhu Hassan leo Jumatatu amehutubia...

error: Content is protected !!