Wednesday , 8 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Polisi Tanzania: Mbowe anatuhumiwa kupanga njama za ugaidi, kuua viongozi wa serikali
Habari za SiasaTangulizi

Polisi Tanzania: Mbowe anatuhumiwa kupanga njama za ugaidi, kuua viongozi wa serikali

Freeman Mbowe, Mwenyekiti wa Chadema
Spread the love

 

JESHI la Polisi nchini Tanzania limesema, linamshikiliwa kiongozi wa chama cha kikuu cha upinzani nchini humo cha Chadema, Freeman Mbowe kwa tuhuma mbalimbali ikiwemo za ugaidi. Anaripoti Mwandishi Wetu…(endelea).

Mbowe na wenzake 14, walikamatwa na Polisi mkoa wa Mwanza, saa 8 usiku wa kuamkia Jumatano tarehe 21 Julai 2021, katika Hotel ya Kingdom, walipokuwa wamefikia.

Siku hiyo, Mbowe alikuwa aongoze kongamano la kudai katiba mpya jijini Mwanza na kujikuta akiishia mikononi mwa polisi. Alisafirishwa jana Jumatano kutoka Mwanza hadi Dar es Salaam.

Leo Alhamisi, tarehe 22 Julai 2021, Msemaji wa Jeshi la Polisi Tanzania, David Misime ametoa taarifa juu ya kushikiliwa kwa Mbowe akisema, alikuwa akichunguzwa juu ya tuhuma mbalimbali.

“…Mbowe anashikiliwa na Jeshi la Polisi kutokana na tuhuma zinazomkabili za kula njama ya kufanya vitendo vya kigaidi ikiwemo kuua viongozi wa serikali ambapo wenzake sita walishafikishwa mahakamani,” amesema Misime

Amesema, uchunguzi unaoendelea Mwanza kutokana na kufanya vitendo vya uvunjifu wa amani, ukibaini kuna sheria aliyovunja, “hatutasita pia kumfikisha mahakamani pamoja na viongozi wenzake wanaoshikiliwa kule.”

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Rais Samia: Matumizi ya nishati safi sio anasa, ladha ipo

Spread the loveRAIS Samia Suluhu Hassan amesema matumizi ya nishati safi kwa...

Habari za SiasaTangulizi

Samia: Kuanzia Agosti marufuku kutumia mkaa, kuni

Spread the loveRAIS Samia Suluhu Hassan amemuagiza Waziri wa Nchi, Ofisi ya...

Habari za SiasaTangulizi

Mwendokasi Kigogo – Segerea kujengwa awamu ya 5

Spread the loveNaibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais (TAMISEMI), Festo Dugange...

Habari za SiasaMakala & Uchambuzi

Rais Samia ni Mzanzibari: Shida Iko Wapi?

Spread the loveTAIFA linakabiliwa na upungufu wa fikra sahihi. Upungufu huu unaonekana...

error: Content is protected !!