Saturday , 25 March 2023
Home Kitengo Michezo Kisa Simba, Yanga wamkataa refa wa Fainali
Michezo

Kisa Simba, Yanga wamkataa refa wa Fainali

Spread the love

 

KLABU ya Yanga imeonekana kusikitishwa na kitendo cha Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) kumchagua Ahmed Arajiga kuwa mwamuzi wa mchezo wao wa fainali dhidi ya Simba kwa madai ya kuwa refa huyo kuchezesha michezo mitatu mfululizo ya wapinzani wao. Anaripoti Kelvin Mwaipungu, Kigoma … (endelea). 

Mchezo huo wa fainali utapigwa siku ya Jumapili Julai 25, Mwaka huu, kwenye Uwanja wa Lake Tanganyika, mjini Kigoma.

Yanga wametoa malalamiko yao ikiwa siku moja tu toka, Shirikisho hilo kuweka hadharani majina ya waamuzi katika mchezo huo wa fainali.

Katika taarifa yao, Yanga wanaamini kuwa Tanzania kuna waamuzi wengi, wenye uwezo hivyo kitendo cha kumrudia mwamuzi moja katika michezo mitatu ya Simba inatia shaka.

Mwamuzi huyo ndiye aliyechezesha mchezo wa hatua ya robo fainali wa kombe hilo, kati ya Simba na Dodoma Jiji na kisha kuchezesha mchezo wa nusu fainali kati ya Simba na Azam Fc ambao ulimalizika kwa Simba kutoka na ushindi wa bao 1-0.

Aidha uongozi wa Yanga umeitaka TFF na kamati ya mashindano kutafakari juu ya maamuzi waliyofanya.

Waamuzi wengine waliopangwa kwenye mchezo huo, ni Frednand Chacha ambaye ni mwamuzi msaidizi namba moja kutoka Mwanza, Mohamed Mkono mwamuzi namba mbili kutooka Tanga, huku mwamuzi wa akiba akiwa ni Elly Sasii kutoka Dar es Salaam.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Michezo

Yanga: Fedha za Rais Samia zinaleta ari kubwa

Spread the loveUONGOZI wa klabu ya Yanga, umesema fedha zinazotolewa na Rais...

Michezo

Simba Sc. yamvulia kofia Rais Samia, yamuahidi makubwa dhidi ya Horoya

Spread the loveWAKATI timu ya Simba ikiibuka na ushindi wa bao 3-0...

Michezo

Taasisi ya TKO na TFF yawapiga msasa makocha wa kike 54

Spread the love WAKATI Soka la wasichana likichipua kwa kasi Taasisi ya...

Michezo

Kimwanga CUP yazidi kutimua vumbi

Spread the loveMASHINDANO ya mpira wa miguu ya Kimwanga CUP ya kuwania...

error: Content is protected !!