Wednesday , 8 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Passport ya Bulaya yaahirisha kesi
Habari za SiasaTangulizi

Passport ya Bulaya yaahirisha kesi

Spread the love

MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Kisutu jijini Dar es salaam, imeahirisha kusikiliza kesi inayowakabili viongozi waandamizi wa Chadema, kutokana na upande wa mashtaka kumtaka mshtakiwa wa tisa, Ester Bulaya, Mbunge wa Bunda Mjini, kuwasilisha mahakamani hapo hati ya kusafiria ili kuendelea kumhoji juu ya ushahidi wake. Anaripoti Faki Sosi … (endelea).

Katika kesi hiyo namba 112 la mwaka 2018, Bulaya anashtakiwa pamoja na viongozi wanane wa chama hicho akiwemo, Freeman Mbowe, Mwenyekiti wa Chadema-Taifa, Vicent Mashinji, Katibu Mkuu Chadema-Taifa, John Mnyika, Naibu Katibu Mkuu Chadema-Bara na Salum Mwalimu, Naibu Katibu Mkuu Chadema-Zanzibar.

Wengine ni Halima Mdee, Mbunge wa Kawe, John Heche, Mbunge wa Tarime Vijijini, Mch. Peter Msigwa, Mbunge wa Iringa Mjini na Ester Matiko, Mbunge wa Tarime Mjini.

Leo tarehe 6 Desemba 2019, Bulaya akiohojiwa na Wakili wa Serikali Mwandamizi, Wankyo Simon ameeleza kuwa tarehe 17 Februari, 2019, alimsindikiza Mdee kwenye hospitali ya St. Parrot nchini Afrika Kusini, kwa ajili ya matibabu.

Bulaya ameulizwa aina gani ya hati ya kusafiria aliyoitumia wakati alipomsindikiza hospitali Mdee amejibu kuwa ni hati ya kawaida.

Wankyo amemuuliza Bulaya iwapo upande wa mashtaka ukiitaka kuiona hati yake kusafiria amejibu kuwa siku yoyote kesi hiyo ikitaja ataiwasilisha.

Wakili wa Serikali Mkuu, Faraja Nchimbi ameiomba mahakama hiyo kuhairisha shauri hilo ili Bulaya akiwasilisha hati ya kusafiria ndipo wataendelea kumhoji.

Hakimu Simba ameahirisha shauri hilo mpaka tarehe 19 na 20 Desemba mwaka huu.

Washtakiwa wote wanatuhumiwa kwa makosa ya kutoa maneno ya uchochezi, kufanya kusanyiko lisilohalali na kufanya maandamano kinyume cha sheria yaliyodaiwa kusababisha kifo cha mwanafunzi wa Chuo cha Taifa cha Usafirishaji (NIT), Akwelina Akwelin.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Rais Samia: Matumizi ya nishati safi sio anasa, ladha ipo

Spread the loveRAIS Samia Suluhu Hassan amesema matumizi ya nishati safi kwa...

Habari za SiasaTangulizi

Samia: Kuanzia Agosti marufuku kutumia mkaa, kuni

Spread the loveRAIS Samia Suluhu Hassan amemuagiza Waziri wa Nchi, Ofisi ya...

Habari za SiasaTangulizi

Mwendokasi Kigogo – Segerea kujengwa awamu ya 5

Spread the loveNaibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais (TAMISEMI), Festo Dugange...

Habari za SiasaMakala & Uchambuzi

Rais Samia ni Mzanzibari: Shida Iko Wapi?

Spread the loveTAIFA linakabiliwa na upungufu wa fikra sahihi. Upungufu huu unaonekana...

error: Content is protected !!