Thursday , 2 May 2024
Home Habari Mchanganyiko Nondo akamatwa tena na Polisi
Habari MchanganyikoTangulizi

Nondo akamatwa tena na Polisi

Abdul Nondo, Mwenyekiti wa Ngome ya Vijana ACT-Wazalendo
Spread the love

MWENYEKITI wa Mtandao wa Wanafunzi nchini (TSNP), Abdull Nondo ametiwa mbaroni na jeshi la Polisi usiku kuamkia leo. Anaripoti Faki Sosi … (endelea).

Akizungumza na MwanaHALISI Online Hellen Sisya Ofisa Habari wa Mtandao huo amethibitisha kushikiliwa kwa kiongozi huyo.

Sisya amesema kuwa Nondo alikamatwa akiwa viunga vya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam usiku wa jana Julai 26 na askari wa chuo hicho.

Paul Kisabo, Mkurugenzi wa Idara ya Sheria wa TSNP, amesema kuwa Nondo amekamatwa akiwa eneo la Mgahawa wa chuo na
askari wa auxiliary.

“Tumefika kituo cha polisi chuo tumekuta Abdul Nondo anachukuliwa maelezo lakini alikataa kuyasaini sababu hakuwa na msaada wa kisheria akiwa anachukuliwa maelezo.

“Sababu ya kukamatwa ni eti amefanya criminal tresspass chuoni, tumeongea na mkuu wa kituo ili tuweze kuondoka na Nondo, imeshindikana kwa sababu za kiusalama,” amesema Kisabo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

NEMC yatoa elimu matumizi sahihi ya zebaki kwa wachimbaji

Spread the loveBARAZA la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC)...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Oryx gesi yagawa mitungi, majiko 100 kwa waandishi wa habari Dar

Spread the loveKAMPUNI ya Oryx Gesi Tanzania imegawa mitungi 100 ya gesi...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mavunde ataja malengo “Vision 2030”

Spread the loveWAZIRI wa Madini amesema dhana ya “Vision 2030” inakusudia kuiendeleza...

Habari MchanganyikoMichezo

Wanamichezo Mei Mosi wachangia wahitaji vitu vya mil. 11.5

Spread the loveWanamichezo wanaoshiriki Michezo ya Mei Mosi Taifa 2024 jijini Arusha...

error: Content is protected !!