Friday , 19 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa ‘CCM inamvua nguo Chiza’
Habari za SiasaTangulizi

‘CCM inamvua nguo Chiza’

Christopher Chiza
Spread the love

CHRISTOPHER Chiza, mgombea mteule wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) katika uchaguzi mdogo wa Jimbo la Buyungu, Kigoma anakwenda kuumbuka. Anaripoti Faki Sosi … (endelea).

“CCM imeamua kumvua nguo Chiza. Kwanza kaishachoka na wananchi wanajua kachoka hoi.

“Kama haki itasimama huku matumizi ya mabavu na uhuni mwingine ukiwekwa kando, Chiza ataanguka mapema.

“Yale ya kuiba masanduku ya kura kule Kinondoni, Dar es Salaam huku hatuyataki, tunaamini Buyungu ni ya amani na wananchi wanataka uchaguzi wa amani. Ni matarajio yetu Chiza ataendelea kupumzika mililele kwenye uso wa dunia,” amesema Elias Michael.

Michael ndio aliyeteuliwa na Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kugombea ubunge kwenye jimbo hilo.

Akizungumza na MwanaHALISI Online Michael amesema kuwa, CCM ni chama pinzani kwenye jimbo hilo kutokana na kuachwa na Mbunge wa Chadema, Kasuku Biloga aliyefariki 26 Mei mwaka huu.

Uchaguzi huo unaotarajiwa kufanyika Agosti 12, 2018 kwenye jimbo la Buyungu sambasamba na kata 79.

Michael amedai, Chiza ni mchovu na hana jipya kwa kuwa, wananchi wanamjua kutokana na kuhudumu jimbo hilo kwa miaka 10.

“Mgombea wa CCM hakuwatendea haki wananchi wa Buyungu wakati akihudumu kama mbunge kwenye awamu ya nne na bahati nzuri alipata nafasi ya kuwa waziri kwa miaka 7 na nafasi ya naibu waziri kwa miaka 3 bila kuwanufaisha wananchi wa Buyungu” amesema Michael.

Michael ambaye ni kijana mbichi kabisa ameeleza kuwa, hasira za wananchi hao zipo kwenye vifua vyao kwa sababu CCM imemrejesha mtu aliyesababisha kuzorota kwa maendelo kwenye jimbo hilo.

Amedai kwamba, wakati Chiza akiwa Waziri wa Kilimo aliwachukiza wananchi wa eneo hilo kwa kuhusika na kuuza pembejeo nchi jirani ya Burundi ihali wananchi wake hawakuwa na mbolea .

Na kwamba, Chiza aliwahi kushindwa kufanikisha mradi wa maji uliogharimu bilioni 2 zilizopotea bila kufanikisha mradi huo.

Michael ameweka wazi kuwa, yeye ni zao la vijana waliosoma kwenye shule za kata na mwenye kujua umuhimu wa elimu hivyo wakati wananchi walipo mkabidhi kijiti cha udiwani ilikuwa ni fursa kwake ya kufanya mabadiliko kwenye kata yake ya Gwarama.

Michael alipoinga kwenye udiwani alikopeshwa shilingi 8 Milioni ambazo zote aliziingiza kwenye ujenzi wa vyumba vinne vya shule ya msingi kwenye kata hiyo ambapo wanafunzi 320 wa Darasa la I na II.

Amesema kuwa, tayari amepatiwa Sh. Mil 60 kutoka Ufaransa kwa ajili ya ujenzi wa Shule ya Sekondari ya Muhange.

Amesema, kwa kipindi cha miaka 3 ya udiwani wake ameshughulikia suala la amani kwenye kata hiyo ambayo hapo awali kulikuwa na matukio ya ujambazi.

“Wananchi wa Buyungu wanajua thamani ya kula zao na nikihujumiwa mimi watahujumiwa wao, kwa hiyo wapiga kura wangu wanajitambua na hawatakubali kunyangwanywa haki yao,” amesema.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

KimataifaTangulizi

Mkuu wa majeshi Kenya afariki, Ruto atangaza maombolezo

Spread the loveRais wa Kenya, William Ruto ametangaza maombezo ya siku tatu...

Habari za Siasa

Tume huru ya uchaguzi yatangaza ajira watendaji daftari wapiga kura

Spread the love  TUME Huru ya Taifa ya Uchaguzi (INEC), imetangaza nafasi...

Habari za SiasaTangulizi

Chadema yatangaza ruti awamu ya pili maandamano

Spread the love  CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimesema awamu ya...

Habari za Siasa

CCM yamkana mwenyekiti UVCCM aliyetaka wapinzani wapotezwe

Spread the love  CHAMA Cha Mapinduzi (CCM), kimejitenga na kauli ya mwenyekiti...

error: Content is protected !!