Thursday , 2 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Ndugai amtisha Heche Tarime Vijijini
Habari za Siasa

Ndugai amtisha Heche Tarime Vijijini

Spread the love

JOB Nduga, Spika wa Bunge la Jamhuri amemtisha John Heche, Mbunge wa Tarime Vijijini kwamba, uchaguzi mkuu ujao jimbo hilo litarudi CCM mapema. Anaripoti Danson Kaijage, Dodoma … (endelea).

Ndugai amesema, kuna ufujaji mkubwa wa miradi ya serikali licha ya mbunge wake kuwa mpinzani na mpiga kelele.

Ameeleza kushangazwa na Heche kwa kushindwa kusimamia miradi ya Sh. 9 Bilioni iliyopo jimboni kwake.

“Ni lazima wabunge tujue miradi iliyo kwenye majimbo yetu,” amesema Ndugai na kuongeza;

“Sasa kama mtu kashindwa kusimamia miradi ya Sh. 9 Bilioni, mwakani atasema nini?”

Ndugai ametoa kauli hiyo leo tarehe 4 Februari 2019 bungeni Dodoma na kudai kwenye uchaguzi mkuu ujao katika jimbo hilo, wimbo utakuwa ni Sh. 9 Bilioni.

Ndugai amedai, kutokana na kushindwa kwa Heche kusimamia, ushindi kwa CCM utakuwa mapema.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mavunde ataja malengo “Vision 2030”

Spread the loveWAZIRI wa Madini amesema dhana ya “Vision 2030” inakusudia kuiendeleza...

Habari za Siasa

Mavunde aomba bilioni 231.9 bajeti wizara ya madini

Spread the loveWAZIRI wa Madini, Anthony Mavunde leo Jumanne amewasilisha hotuba ya...

Habari za SiasaTangulizi

Lissu amjibu Fatma Karume kuhusu Rais Samia

Spread the love  MAKAMU Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema)...

Habari za SiasaTangulizi

Dk. Slaa: Watanzania iungeni mkono Chadema uchaguzi 2025

Spread the loveMWANASIASA mkongwe nchini Tanzania, Dk. Wilbroad Slaa, amewataka watanzania wakiunge...

error: Content is protected !!