Saturday , 27 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Mwanamichezo ajitosa Urais Zanzibar
Habari za Siasa

Mwanamichezo ajitosa Urais Zanzibar

Spread the love

HASHIM Salum Hashim, Mjumbe wa Kamati Tendaji ya Chama cha Mpira wa Miguu Zanzibar (ZFA), amejitosa katika kinyang’anyiro cha Urais wa Zanzibar, kupitia Chama cha Mapinduzi (CCM). Anaripoti Mwandishi Wetu, Zanzibar … (endelea).

Leo Jumanne tarehe 23 Juni 2020 katika Ofisi Kuu ya CCM Zanzibar iliyoko Kisiwandui, Hashim amekabidhiwa fomu ya kuwania nafasi ya kugombea urais Zanzibar na Cassian Gallo’s, Katibu wa Kamati Maalumu ya NEC, Idara ya Oganaizesheni Zanzibar.

Akizungumza baada ya kukabidhiwa fomu hiyo, amesema kama atafanikiwa kuwa Rais wa Zanzibar, ataiboresha sekta ya michezo visiwani humo pamoja na kurejesha hashima ya Zanzibar kimataifa.

Hashim amesema, endapo atafanikiwa kuwa Rais wa Zanzibar, atahakikisha taifa hilo linapata uanachama kamili katika Shirikisho la Mpira wa Miguu Barani Afrika (CAF) na Shirikisho la Mpira wa Miguu Duniani (FIFA).

Hamad Masauni, Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani wa Tanzania akichukua fomu ya kugombea Urais wa Zanzibar kwa tiketi ya CCM

“Kutokana na uzoefu niliokuwa nao nitahakikisha heshima ya Zanzibar inarudi, tunapata uanachama kamiliwa FIFA na CAF,” amesema Hashim.

Wakati huo huo, Hashim amesema kutokana na uzoefu aliokuwa nao kwenye masuala ya michezo, “Nitahakikisha michezo itapata udhamini wa Asilimia 100 kutoka serikalini sababu mpaka sasa Ligi Kuu Zanzibar inacheza haina mdhamini. Ni wajibu wangu kama mwanamichezo nitahakikisha udhamini unapatikana na michezo inatoa ajira.”

“Kwa hiyo nitahakikisha udhamini unarudi na michezo yote inapata wadhamini sababu vipaji vipo shida ni umasikini tu, uwezo wa kupata CAF tunao na wa kupata FIFA tunao,” amesema

Hashim ambaye amekuwa mwanachama wa 24 wa CCM kuchukua fomu ya kugombea urais wa Zanzibar, ameahidi kwamba, kama chama chake kitamteua kugombea urais na kushinda, ataendelea mazuri aliyoyafanya Dk. Ali Shein, Rais anayemaliza muda wake.

Amesema ataendeleza pale alipoacha Rais Shein, kwenye siasa, afya, elimu na miundombinu.

 “Kama chama kikinipa ridhaa ya kupeperusha bendera, nitaanza pale alipoachia Rais Shein katika siasa uchumi, elimu na mambo mengine, na masuala mazima ya michezo,” amesema Hashim.

Wengine 23 waliokwisha kuchukua fumo ni;

  1. Mbwana Bakari Juma
  2. Ali Abeid Karume
  3. Mbwana Yahya Mwinyi :
  4. Omar Sheha Mussa
  5. Hussein Ali Mwinyi
  6. Shamsi Vuai Nahodha
  7. Mohammed Jaffar Jumanne
  8. Mohammed Hijja Mohammed
  9. Issa Suleiman Nassor
  10. Makame Mnyaa Mabarawa
  11. Mwatum Mussa Sultan
  12. Haji Rashid Pandu
  13. Abdulhalim Mohammed Ali
  14. Jecha Salum Jecha
  15. Dk Khalid Salum Mohammed
  16. Rashid Ali Juma
  17. Khamis Mussa Omar
  18. Mmanga Mjengo Mjawiri
  19. Hamad Yussuf Masauni
  20. Mohammed Aboud Mohammed
  21. Bakari  Rashid Bakari
  22. Hussein Ibrahim Makungu
  23. Ayoub Mohammed Mahmoud 

Endelea kufuatilia MwanaHALISI ONLINE & MwanaHALISI TV kwa habari zaidi

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Sauti ya Watanzania waeleza sababu za kuiunga mkono Chadema

Spread the love  KIKUNDI kinachojipambanua katika kupigania rasilimali na uhuru wa nchi,...

Habari za SiasaKimataifaTangulizi

Tanzania, Somalia kuibua maeneo mapya ya ushirikiano

Spread the love  RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amesema Tanzania na Somalia...

Habari za Siasa

ACT: Waongoza watalii wapate maslahi yao inavyostahili

Spread the loveCHAMA cha ACT-Wazalendo kimeitaka serikali kuhakikisha inasimamia maslahi stahiki ya...

Habari za SiasaTangulizi

Prof. Lipumba ajitosa kuviunganisha vyama vya siasa Burundi

Spread the love  MWENYEKITI wa Kituo Cha Demokrasia Tanzania (TCD), Prof. Ibrahim...

error: Content is protected !!