Monday , 11 December 2023
Home Kitengo Maisha Elimu Mtwara Girls waondokana na changamoto ya maji
ElimuHabari Mchanganyiko

Mtwara Girls waondokana na changamoto ya maji

Spread the love

 

WANAFUNZI wa Shule ya Sekondari ya Wasichana mkoani Mtwara (Mtwara Girls High School), wameishukuru Serikali ya Rais Dk. Samia Suluhu Hassan, kwa kuwaondolea changamoto ya uhaba wa maji iliyodumu shuleni hapo kwa muda mrefu. Anaripoti Mwandishi Wetu, Mtwara … (endelea).

Shukrani hizo zimetolewa na wanafunzi hao, baada ya huduma ya maji ya uhakika kurejea shuleni hapo kufuatia hatua ya Rais Samia kuzindua chujio la maji katika mradi wa Mangamba.

Sekondari ya Mtwara Girls ni miongoni mwa wanufaika wa mradi huo uliozinduliwa rasmi na Rais Samia katika ziara yake ya kikazi kwenye mikoa ya kusini, aliyofanya hivi karibuni.

Rais Samia Suluhu Hassan

Akizungumza kwa niaba ya wanafunzi wenzake, Farida Twaha amesema “tunafurahia huu mradi mpya uliozinduliwa na Rais Samia, umesaidia kutatua changamoto ya maji iliyokuwepo muda mrefu. Kabla ya mradi kuzinduliwa kulikuwa na changamoto ya maji.”

Farida amesema, upatikanaji wa maji safi na salama utawasaidia kukidhi mahitaji yao ya kila siku, kutokana na watoto wa kike kuwa na uhitaji mkubwa.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Amsons Group watoa milioni 100 waathirika maafa Hanang

Spread the loveKAMPUNI ya Amsons Group kupitia kampuni zake za Camel Oil...

Habari Mchanganyiko

Kesi ya mfanyakazi wa CRDB itaendelea J’tatu

Spread the love  MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Kinondoni, Dar es Salaam inatarajia...

Habari Mchanganyiko

Mawasiliano Dar – Bagamoyo yarejea

Spread the loveMAWASILIANO ya barabara ya Mkoa wa Pwani na Dar es...

ElimuTangulizi

Mwalimu Maganga Japhet asimamishwa kazi kwa utoro

Spread the loveMwalimu Maganga Japhet amesimamishwa kazi na Tume ya Utumishi wa...

error: Content is protected !!