Saturday , 27 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Msuya awataka viongozi CCM kuisimamia serikali
Habari za Siasa

Msuya awataka viongozi CCM kuisimamia serikali

Hemed Msuya
Spread the love

Viongozi wa Chama Cha Mapinduzi wilayani Kilombero, wametakiwa kuisimamia serikali ili iendelee kutekeza ilani ya uchaguzi ya chama hicho ipasavyo. Anaripoti Victor Makinda, Morogoro … (endelea).

Agizo hilo limetolewa na Mwenyekiti wa CCM, Wilaya ya Kilombero,  Hemed Msuya, wakati wa sherehe za maadhimisho ya miaka 47 ya kuzaliwa kwa CCM, yaliyofanyika kwa ngazi ya wilaya  Kata ya Msolwa Steheni, Wilayani Kilombero, Mkoani Morogoro jana.

Mjumbe wa Kamati ya Siasa ya CCM, Wilaya ya Kilombero, akizungumza jambo wakati wa maadhimisho ya miaka 47 ya chama hicho.

Msuya amesema CCM ndiyo chama kilichopata ridhaa ya wananchi ya kuunda serikali kupitia sanduku la kura, hivyo viongozi wa chama hicho wana dhima  ya kuwasimamia watendaji wa serikali na kuwawajibisha viongozi wote wanaoendekeza  urasimu na  ugoi goi katika kuwahudumia wananchi.

“Msiogope, chama ni zaidi ya serikali, kipo juu na serikali ipo chini ya chama. Mjitambue kuwa ninyi ni wasimamizi wa kuwasimamia viongozi wa serikali ili wafanye kazi kwa bidiii kutekeleza ilani ya CCM,” alisema Msuya.

Exif_JPEG_420

Aliongeza kusema kuwa CCM wilayani Kilombero, haitasita kuwachukulia hatua watendaji wa serikali wasiotimiza wajibu  wao wa kuwahudumia wananchi.

Akizungumza kuhusu miaka 47 tangu kuzaliwa kwa CCM, Msuya amesema kuwa chama hicho kinajivuni misingi iliyoasisi na kuilinda, ikiwa ni uzalendo, utu, umoja na mshikamano wa kitaifa.

Naye Mwenyekiti wa Halmashauri ya Ifakara Mji, wilaya ya Kilombero, Kasim Nakapala, akizungumza kwenye maazimisho hayo, alisema kuwa wakati tunasherehekea miaka 47 ya CCM, Halmashauri ya Kilombero imepokea miradi mingi ya maendeleo hivyo ni wajibu wa watendaji wote wa serikali kusimamia miradi hiyo ili ilete tija kwa wananchi.

“Tunaimshukuru serikali ya awamu ya sita, chini ya uongozi wa Rais Samia Suluhu Hassan, kwa kutuletea miradi mingi ya maendeleo wilayani kilombero, ikiwa ni miradi ya elimu, afya,kilimo, umeme na ujenzi wa barabara, hivyo watendaji wa serikali wanapaswa kuendana na kasi ya rais katika kusimamia miradi hiyo ili ituletee maendeleo,”alisema Nakapala.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Sauti ya Watanzania waeleza sababu za kuiunga mkono Chadema

Spread the love  KIKUNDI kinachojipambanua katika kupigania rasilimali na uhuru wa nchi,...

Habari za SiasaKimataifaTangulizi

Tanzania, Somalia kuibua maeneo mapya ya ushirikiano

Spread the love  RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amesema Tanzania na Somalia...

Habari za Siasa

ACT: Waongoza watalii wapate maslahi yao inavyostahili

Spread the loveCHAMA cha ACT-Wazalendo kimeitaka serikali kuhakikisha inasimamia maslahi stahiki ya...

Habari za SiasaTangulizi

Prof. Lipumba ajitosa kuviunganisha vyama vya siasa Burundi

Spread the love  MWENYEKITI wa Kituo Cha Demokrasia Tanzania (TCD), Prof. Ibrahim...

error: Content is protected !!