Thursday , 2 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Msitu wa wanaCCM Nkenge haunitishi – ‘mgombea’ Chadema
Habari za Siasa

Msitu wa wanaCCM Nkenge haunitishi – ‘mgombea’ Chadema

Hilda Rweikila, aliyekuwa Diwani wa Viti Maalum (Chadema)
Spread the love

JIMBO la Nkenge lililopo katika Wilaya ya Misenye, Kagera linawindwa na makada 19 wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) na mmoja kutoka Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema). Anaripoti Danson Kaijage, Kagera … (endelea).

Mpaka sasa, Hilda Rweikila, aliyekuwa Diwani wa Viti Maalum (Chadema), ndio mwanachama wa Chadema aliyejitosa kuwania jimbo hilo huku akisema, ‘CCM hawaaminiani, ndio maana kila mmoja analitaka jimbo.’

Balozi Dk. Diodorus Kamala, anayemaliza muda wake (CCM), ni miongoni mwa watia nia 20 kwenye jimbo hilo.

Hilda anatajwa kuwa na ushawishi kwenye jimbo hilo kutokana na uzoefu na umaarufu wake kisiasa.

Akizungumza na MwanaHALISI Online, Hilda amesema, amesukumwa kuchukua fomu ili ndoto ya wana Nkenge iliyoshindwa kufikiwa kwa miaka mitano iliyopita, aibebe kuelekea mafanikio hayo.

“Mimi sina kipato kikubwa lakini nina msimamo wa kuwatetea watu, na siyo kwamba sijatishwa kugombea, nimetishwa sana na wakati mwingine walikuwa hawanishirikishi vikao mbalimbali hasa vikao vya Kamati ya Fedha.

“…lakini nilikomaa nao, sikuogopa vitisho wala nini na ndiyo maana nimelazimika kuchukua fomu ili chama kikinipa ridhaa ya kugombea, niweze kupata uwanja mpana wa kuwatetea na kupeleka hoja zao bungeni,” anasema Hilda.

Anasema, tangu aanze kupiga kura, hajawahi kuipigia CCM na zaidi, wabunge wanaopatikana katika jimbo hilo, hawana msaada kwa wanachi.

Amesema, siasa ni mapambano hivyo hakuna sababu yoyote ya kuogopa kuwapambania watu ambao wanaohitaji mabadiliko.

Hilda akitumia msemo uliozoeleka kwa Wahaya kuwa waliohama wamekula “mandazi,” kwa maana ya kuhongwa anasema, watu wa aina hiyo ni wenye tamaa.

Awali, Jimbo la Nkenge liliwahi kuongozwa na aliyekuwa Mkuu wa Wilaya ya Kibaha, Assumpter Mshama ambaye alishindwa na Dk. Kamala.

1 Comment

  • Nawashauri Bukoba Vijijini chagueni MwanaCCM mwingine si huyo tuliyenaye.

    Na nyie wa Misenyi,kwa mini mlimpiga chini Mama Asumpta?Mbona Serikali ilimuona DILI ikampa U-DC?
    Anarudi mpokeeni.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mavunde ataja malengo “Vision 2030”

Spread the loveWAZIRI wa Madini amesema dhana ya “Vision 2030” inakusudia kuiendeleza...

Habari za Siasa

Mavunde aomba bilioni 231.9 bajeti wizara ya madini

Spread the loveWAZIRI wa Madini, Anthony Mavunde leo Jumanne amewasilisha hotuba ya...

Habari za SiasaTangulizi

Lissu amjibu Fatma Karume kuhusu Rais Samia

Spread the love  MAKAMU Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema)...

Habari za SiasaTangulizi

Dk. Slaa: Watanzania iungeni mkono Chadema uchaguzi 2025

Spread the loveMWANASIASA mkongwe nchini Tanzania, Dk. Wilbroad Slaa, amewataka watanzania wakiunge...

error: Content is protected !!