Sunday , 28 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Mpina aibana Serikali kuadimika kwa dola
Habari za Siasa

Mpina aibana Serikali kuadimika kwa dola

Luhaga Mpina
Spread the love

MBUNGE wa Kisesa, ameihoji Serikali sababu za Dola za Marekani kuadimika nchini, wakati ikijinasibu kwamba kuna ongezeko la uwekezaji, utalii na mauzo ya nje. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dodoma…(endelea).

Mpina amehoji hayo leo tarehe 31 Agosti 2023, bungeni jijini Dodoma, akichangia hoja ya Waziri wa Viwanda na Biashara, Ashatu Kijaji, ya Bunge kuridhia Itifaki ya Biashara ya Huduma ya Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) ya 2012.

Alihoji hayo wakati akieleza umuhimu wa uwepo wa Dola za Marekani za kutosha, wakati Tanzania ikiridhia itifaki hiyo yenye lengo la kukuza ushirikiano wa nchi wanachama wa SADC katika biashara na sekta mbalimbali.

“Tunazungumzia ushirikiano wa sekta ya fedha nchini, hata SADC tunategemea dola na hamna zimeadimika. Wafanyabiashara hawapati dola hawawezi kuagiza mizigo sasa tunafanyaje? Maelezo yanayotolewa na Serikali ni kwamba utalii umeongezeka, uwekezaji umeongezeka maradufu sasa dola zimeenda wapi?” amehoji Mpina na kuongeza:

“Serikali lazima itatue tatizo la kuadimika kwa dola na hasa mimi ninavyoona sababu ziko nyingi zilizopelekea dola kuadimika.”

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Sauti ya Watanzania waeleza sababu za kuiunga mkono Chadema

Spread the love  KIKUNDI kinachojipambanua katika kupigania rasilimali na uhuru wa nchi,...

Habari za SiasaKimataifaTangulizi

Tanzania, Somalia kuibua maeneo mapya ya ushirikiano

Spread the love  RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amesema Tanzania na Somalia...

Habari za Siasa

ACT: Waongoza watalii wapate maslahi yao inavyostahili

Spread the loveCHAMA cha ACT-Wazalendo kimeitaka serikali kuhakikisha inasimamia maslahi stahiki ya...

Habari za SiasaTangulizi

Prof. Lipumba ajitosa kuviunganisha vyama vya siasa Burundi

Spread the love  MWENYEKITI wa Kituo Cha Demokrasia Tanzania (TCD), Prof. Ibrahim...

error: Content is protected !!