MBUNGE wa Kisesa, ameihoji Serikali sababu za Dola za Marekani kuadimika nchini, wakati ikijinasibu kwamba kuna ongezeko la uwekezaji, utalii na mauzo ya nje. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dodoma…(endelea).
Mpina amehoji hayo leo tarehe 31 Agosti 2023, bungeni jijini Dodoma, akichangia hoja ya Waziri wa Viwanda na Biashara, Ashatu Kijaji, ya Bunge kuridhia Itifaki ya Biashara ya Huduma ya Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) ya 2012.
Alihoji hayo wakati akieleza umuhimu wa uwepo wa Dola za Marekani za kutosha, wakati Tanzania ikiridhia itifaki hiyo yenye lengo la kukuza ushirikiano wa nchi wanachama wa SADC katika biashara na sekta mbalimbali.
“Tunazungumzia ushirikiano wa sekta ya fedha nchini, hata SADC tunategemea dola na hamna zimeadimika. Wafanyabiashara hawapati dola hawawezi kuagiza mizigo sasa tunafanyaje? Maelezo yanayotolewa na Serikali ni kwamba utalii umeongezeka, uwekezaji umeongezeka maradufu sasa dola zimeenda wapi?” amehoji Mpina na kuongeza:
“Serikali lazima itatue tatizo la kuadimika kwa dola na hasa mimi ninavyoona sababu ziko nyingi zilizopelekea dola kuadimika.”
Leave a comment