MAKAMU wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar, Othman Masoud Othman yeye pamoja na Serikali ya Mapinduzi Zanzibar wako tayari kushirikiana na wawekezaji, Serikali zote na wadau wote ili rasilimali zilizopo zitumike kwa manufaa ya watu wote. Anaripoti Isaya Temu …(endelea).
Othman ametoa kauli hiyo leo tarehe 31 Agosti 2023 wakati akitoa salamu za Serikali ya ya Mapinduzi Zanzibar kwa Rais Samia Suluhu Hassan katika hafla ya kufunga Tamasha la Kizimkazi ambalo limefanyika kwa sikua tano mfululio kwenye viwanja vya Paje, Mkoa wa Kusini Visiwani Zanzibar.
Pia amesema Serikali itaendelea kushirikiana na wadau wote katika kuenzi hili tamasha hilo na kuhakikisha vivutio na rasilimali zinazopatikana katika Mkoa huo na Zanzibar kwa ujumla zinatumika kwa manufaa ya wananchi wote.
Makamu huyo amesema licha ya mkoa huo kuwa mkubwa Visiwani Zanzibar ukiwa na kilomita za mraba 811, una idadi ndogo ya watu lakini pia ndio mkoa wenye vivutio vingi ikiwemo eneo la Makumbusho la Kizimkazi.
Pia amesema mkoa huo una Msitu wa Juzani ambao umepewa hadhi ya Kimataifa ya “biosphere reserve” ambazo kwa Tanzania ziko tano.
Amesema kuwa pamoja na kuwa na vivutio vyote hivyo bado hali ya maisha ya watu katika maeneo hayobado ni duni.
“Tunajiuliza kama tuna vivutio vyote hivyo, lakini bado tuna njaa” alisema Othman.
Hata hivyo, Makamu huyo amesema kuwa Rais Samia ameonyesha kuwa viongozi wanaweza kutenda vizuri zaidi kutumia rasilimali hizo kufaidisha watu.
“Leo umekuja kutuonesha ni namna gani tunaweza kutumia rasilimali hizi na tukashiba tukaenda upweo,” aliongeza Othman.
Leave a comment