Friday , 3 May 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa Mmoja afariki, 13 wajeruhiwa vibaya Korea Kusini
Kimataifa

Mmoja afariki, 13 wajeruhiwa vibaya Korea Kusini

Spread the love

KIJANA mmoja anayekadiriwa kuwa na umri wa miaka 20 amewashambulia watu 14 kwa kuwagonga na gari na kuwachoma kwa kutumia kitu chenye ncha kali na kusababishia kifo na majeraha katika jiji la Seongnam karibu na mji  mkuu Seol nchini Korea Kusini. Anaripoti Isaya Temu, TUDARCo … (endelea). 

Mshukiwa huyo aliendesha  gari lake hovyo na kuwagonga  watu watano, kisha alishuka na kuwachoma visu watu wengine tisa katika kituo cha ununuzi chenye shughuli nyingi ambapo mwanaume mmoja anayekadiriwa kuwa na umri wa miaka 60 akifariki dunia baada ya shambulio hilo.

Mashuhuda wa tukio hilo, wameeleza kuwa walimuona kijana huyo akiwa amevalia mavazi yote meusi pamoja na miwani nyeusi huku akiwa amebeba kisu mkononi mwake na ndicho alichotumia kuwashambulia wahanga baada ya kushuka kwenye gari.

“Ghafla, mtu mmoja alituambia kwamba mtu aliyetenda kosa alikuwa akija kwenye ghorofa ya pili, hivyo tukakimbia kwa hofu,” alieleza shuhuda wa shambulizi hilo huku akiongeza kuwa baada ya taarifa hiyo watu wengine walijificha katika jokofu kwa hofu.

Polisi wa eneo hilo walifanya jitihada na kufanikiwa kumkamata kijana huyo dakika 10 baada ya taarifa kusambazwa na uchunguzi juu ya tukio hilo unaendelea. 

“Watu tisa walichomwa kisu katika eneo hilo, huku wengine watano wakijeruhiwa baada ya mshukiwa kuendesha gari kwenye njia ya watembea kwa miguu kabla ya shambulio la kisu”, alisema Lee Ki-in, afisa wa serikali ya Mkoa wa Gyeonggi, katika taarifa kwenye Facebook.

Majeruhi wa tukio hilo walikimbizwa hospitalini kwa ajili ya matibabu ya haraka kwani wengi wa majeruhi walikuwa na hali mbaya.

Viongozi walijadili kuongeza doria za usiku katika maeneo ya starehe na mengine yenye watu wengi na kuimarisha ufuatiliaji wa kamera za usalama.

Mwezi uliopita, mtu aliyekuwa na visu aliwadunga kisu angalau watembea kwa miguu wanne kwenye barabara katika mji mkuu Seoul.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaKimataifa

Mwanamke Rwanda ataka kupambana tena na Kagame

Spread the loveKIONGOZI wa kihistoria wa upinzani nchini Rwanda, Victoire Ingabire Umuhoza,...

Habari MchanganyikoKimataifa

Ruto amteua Kahariri kuwa mkuu wa majeshi

Spread the loveRAIS wa Kenya, William Ruto, amemteua Jenerali Charles Muriu Kahariri,...

Habari za SiasaKimataifaTangulizi

Tanzania, Somalia kuibua maeneo mapya ya ushirikiano

Spread the love  RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amesema Tanzania na Somalia...

KimataifaTangulizi

Mkuu wa majeshi Kenya afariki, Ruto atangaza maombolezo

Spread the loveRais wa Kenya, William Ruto ametangaza maombezo ya siku tatu...

error: Content is protected !!