RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk. Samia Suluhu Hassan atakuwa mgeni Rasmi katika Tamasha la Michezo Simba Day litakalofanyika Jumapili ya tarehe 6 Agosti, 2023 kwenye Uwanja wa Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Anaripoti Isaya Temu, TURDARCo … (endelea).
Kupitia machapisho yao katika mitandao ya kijamii klabu ya Simba wameandika “Karibu kwenye kilele cha Wiki ya Simba. Karibu kwenye Simba Day, Mheshimiwa Rais Dk. Samia Suluhu Hassan (@SuluhuSamia). Hii ni siku muhimu kwa Klabu ya Simba na wapenda michezo wote nchini Tanzania.
Karibu kwenye kilele cha Wiki ya Simba. Karibu kwenye Simba Day, Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan (@SuluhuSamia). Hii ni siku muhimu kwa Klabu ya Simba na wapenda michezo wote nchini Tanzania.
Tunakushukuru na tanakukaribisha kwa furaha kubwa isiyo na kifani. Kwa… pic.twitter.com/CTqZMV4qxl
— Simba Sports Club (@SimbaSCTanzania) August 4, 2023
Tunakushukuru na tanakukaribisha kwa furaha kubwa isiyo na kifani. Kwa kipekee kabisa, tunakushukuru sana kwa mchango wako mkubwa kwenye sekta ya Michezo na Maendeleo ya Taifa kwa ujumla. Karibu sana Mheshimiwa Rais”.
Tarehe 06.08.2023 ni kilele cha wiki ya Simba Day na muendelezo wa matamasha yao ya kila mwaka ambayo hutumia kujumuika na washabiki wao, kutambulisha wachezaji wapya, benchi la ufundi, malengo na matarajio yao kuelekea msimu mpya.
Leave a comment