NIMROD Elirehema Mkono, aliyekuwa mbunge wa Musoma Vijijini na baadaye Butiama, kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), amefariki dunia leo Jumanne nchini Marekani. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).
Mkono alikuwa Marekani tangu mwaka 218, alikokwenda kupatiwa matibabu ya tatizo la kusahau.
Taarifa za kifo cha Mkono, zimethitishwa na mdogo wake Zadock Mkono ambaye amesema taarifa zaidi kuhusu sababu za kifo cha kaka yake na taratibu nyingine zitatolewa baadaye.
Mwanasiasa huyo ambaye alikuwa wakili mashuhuri nchini, alikuwa miongoni kwa wanasiasa na wanasheria waliowahi kutuhumiwa kwa ufisadi na chama Kikuu Cha upinzani cha CHADEMA, Septemba 2007.
Bwana alitoa na ametwaa..! Na raha ya milele umpe eeh. Bwana.. Amina