Sunday , 3 December 2023
Home Gazeti Habari za Siasa Membe achukua fomu kuwania urais Tanzania
Habari za Siasa

Membe achukua fomu kuwania urais Tanzania

Spread the love

BERNARD Kamilius Membe, Mgombea Urais wa Tanzania kupitia chama cha ACT-Wazalendo, amechukua fomu ya kuwania urais katika Uchaguzi Mkuu utakaofanyika Jumatano tarehe 28 Oktoba 2020. Anaripoti Mwandishi Wetu…(endelea)

Membe ambaye ni Mshauri Mkuu wa chama hicho, amekabidhiwa fomu hizo leo Ijumaa tarehe 7 Agosti 2020, Ofisi za Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) jijini Dodoma na Mwenyekiti wa Tume hiyo, Jaji mstaafu Semistocles Kaijage

Membe aliyewahi kuwa waziri wa mambo ya nje wa Tanzania katika utawala uliopita chini ya Rais mstaafu Jakaya Mrisho Kikwete aliongozana na mgombea mwenza, Profesa Omar Fakih Hamad.

          Soma zaidi:-

Pia, wamesindikizwa na viongozi wa chama hicho, Maalim Seif Sharif Hamad (mwenyekiti) na Katibu Mkuu wake, Ado Shaibu.

Juzi Jumatano, mkutano mkuu wa ACT-Wazalendo ulimteua Membe kugombea urais kwa kupata kura 410 sawa na asilimia 97 ya kura zote 420. Kura za wajumbe 10 zilimkataa.

Shughuli ya uchukuaji na urejeshaji wa fomu hizo ulianza tarehe 5 utahitimishwa 25 Agosti 2020.

Kampeni za uchaguzi mkuu zitaanza 26 Agosti hadi 27 Oktoba 2020 na Uchaguzi Mkuu utafanyika Jumatano tarehe 28 Oktoba 2020.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Dk. Biteko aagiza wakurugenzi TANESCO kukemea rushwa kwenye maeneo yao

Spread the loveNaibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto Biteko...

Habari za SiasaMakala & Uchambuzi

Uongozi wa Samia kuendelea hadi 2030

Spread the loveKWETU sisi tuliowahi kusoma sekondari, iwe O levo au A...

Habari za SiasaMakala & Uchambuzi

Bado askari wastaafu wanaonewa

Spread the loveRAIS wangu Samia Suluhu Hassan tunaendelea kumshukuru Mungu kwamba wote...

Habari za SiasaMakala & Uchambuzi

Tunastawisha ufisadi na kuchukia matunda yake

Spread the loveBUNGE la Jamhuri linaloendelea mjini Dodoma, kwa wiki nzima limetawaliwa...

error: Content is protected !!