Thursday , 2 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Membe achukua fomu kuwania urais Tanzania
Habari za Siasa

Membe achukua fomu kuwania urais Tanzania

Spread the love

BERNARD Kamilius Membe, Mgombea Urais wa Tanzania kupitia chama cha ACT-Wazalendo, amechukua fomu ya kuwania urais katika Uchaguzi Mkuu utakaofanyika Jumatano tarehe 28 Oktoba 2020. Anaripoti Mwandishi Wetu…(endelea)

Membe ambaye ni Mshauri Mkuu wa chama hicho, amekabidhiwa fomu hizo leo Ijumaa tarehe 7 Agosti 2020, Ofisi za Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) jijini Dodoma na Mwenyekiti wa Tume hiyo, Jaji mstaafu Semistocles Kaijage

Membe aliyewahi kuwa waziri wa mambo ya nje wa Tanzania katika utawala uliopita chini ya Rais mstaafu Jakaya Mrisho Kikwete aliongozana na mgombea mwenza, Profesa Omar Fakih Hamad.

          Soma zaidi:-

Pia, wamesindikizwa na viongozi wa chama hicho, Maalim Seif Sharif Hamad (mwenyekiti) na Katibu Mkuu wake, Ado Shaibu.

Juzi Jumatano, mkutano mkuu wa ACT-Wazalendo ulimteua Membe kugombea urais kwa kupata kura 410 sawa na asilimia 97 ya kura zote 420. Kura za wajumbe 10 zilimkataa.

Shughuli ya uchukuaji na urejeshaji wa fomu hizo ulianza tarehe 5 utahitimishwa 25 Agosti 2020.

Kampeni za uchaguzi mkuu zitaanza 26 Agosti hadi 27 Oktoba 2020 na Uchaguzi Mkuu utafanyika Jumatano tarehe 28 Oktoba 2020.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mavunde ataja malengo “Vision 2030”

Spread the loveWAZIRI wa Madini amesema dhana ya “Vision 2030” inakusudia kuiendeleza...

Habari za Siasa

Mavunde aomba bilioni 231.9 bajeti wizara ya madini

Spread the loveWAZIRI wa Madini, Anthony Mavunde leo Jumanne amewasilisha hotuba ya...

Habari za SiasaTangulizi

Lissu amjibu Fatma Karume kuhusu Rais Samia

Spread the love  MAKAMU Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema)...

Habari za SiasaTangulizi

Dk. Slaa: Watanzania iungeni mkono Chadema uchaguzi 2025

Spread the loveMWANASIASA mkongwe nchini Tanzania, Dk. Wilbroad Slaa, amewataka watanzania wakiunge...

error: Content is protected !!