Friday , 29 March 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Magufuli achukua fomu kuwania urais Tanzania
Habari za SiasaTangulizi

Magufuli achukua fomu kuwania urais Tanzania

Spread the love

DAKTARI John Pombe Magufuli amechukua fomu ya kuwania urais wa nchi hiyo kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM) leo Alhamisi tarehe 6 Agosti 2020 katika Ofisi za Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) zilizopo Ndejengwa jijini Dodoma. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dodoma … (endelea).

Magufuli ambaye ni Rais wa Tanzania, ameambatana na mgombea mwenza, Samia Suluhu Hassa na viongozi mbalimbali wa CCM akiwemo Dk. Bashiru Ally, katibu mkuu wa chama hicho na Waziri Mkuu wa Tanzania, Kassim Majaliwa.

Magufuli amekabidhi fomu hizo na Jaji Semistocles Kaijage, Mwenyekiti wa NEC kwa gharama ya Sh.1 milioni.

Magufuli amekuwa mgombea wan ne wa nafasi hiyo kuchukua fomu akitanguliwa na, Seif Maalim Seif wa Chama cha Alliance for African Farmers Party (AAFP), Philipo John Fumbo wa Chama cha Democratic Party (DP) na Leopold Mahona wa Chama cha National Reconstruction Alliance (NRA).

 

Shughuli ya uchukuaji na urejeshaji wa fomu, umeanza jana Jumatano hadi tarehe 25 Agosti 2020 siku ambayo utafanyika uteuzi.

Tarehe 26 Agosti hadi 27 Oktoba 2020 kitakuwa kipindi cha kampeni na Jumatano 28 Oktoba 2020 itakuwa ni siku ya upigaji kura.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaMakala & Uchambuzi

Nani anasema kuna hasara ATCL?

Spread the loveRIPOTI za makusanyo na matumizi ya fedha katika Kampuni ya...

Habari za SiasaTangulizi

CAG: Wastaafu, wenza wao chanzo NHIF kufilisika

Spread the loveRIPOTI ya ukaguzi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu...

Habari za SiasaTangulizi

Vikundi hewa 851 vyalamba bilioni 2.6 mikopo ya halmashauri

Spread the loveVIKUNDI hewa vya wajasirimali wadogo 851 kutoka katika halmashauri 19...

Habari za SiasaTangulizi

Mashirika matano yapata hasara mabilioni ya fedha

Spread the loveMASHIRIKA matano ya Serikali yanayojiendesha kibiashara, yamepata hasara ya mabilioni...

error: Content is protected !!