DAKTARI John Pombe Magufuli amechukua fomu ya kuwania urais wa nchi hiyo kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM) leo Alhamisi tarehe 6 Agosti 2020 katika Ofisi za Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) zilizopo Ndejengwa jijini Dodoma. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dodoma … (endelea).
Magufuli ambaye ni Rais wa Tanzania, ameambatana na mgombea mwenza, Samia Suluhu Hassa na viongozi mbalimbali wa CCM akiwemo Dk. Bashiru Ally, katibu mkuu wa chama hicho na Waziri Mkuu wa Tanzania, Kassim Majaliwa.
Magufuli amekabidhi fomu hizo na Jaji Semistocles Kaijage, Mwenyekiti wa NEC kwa gharama ya Sh.1 milioni.
Magufuli amekuwa mgombea wan ne wa nafasi hiyo kuchukua fomu akitanguliwa na, Seif Maalim Seif wa Chama cha Alliance for African Farmers Party (AAFP), Philipo John Fumbo wa Chama cha Democratic Party (DP) na Leopold Mahona wa Chama cha National Reconstruction Alliance (NRA).
Shughuli ya uchukuaji na urejeshaji wa fomu, umeanza jana Jumatano hadi tarehe 25 Agosti 2020 siku ambayo utafanyika uteuzi.
Tarehe 26 Agosti hadi 27 Oktoba 2020 kitakuwa kipindi cha kampeni na Jumatano 28 Oktoba 2020 itakuwa ni siku ya upigaji kura.
Leave a comment