MBUNGE Viti Maalum, Halima Mdee (Chadema), ametishia kutopitisha fungu lenye bajeti ya mashahara wa Waziri wa Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, George Simbachawene, endapo hatatoa majibu ya kuridhisha kuhusu muarobaini wa madai ya watumishi wa umma. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dodoma … (endelea).
Tukio hilo limetokea leo tarehe 20 Aprili 2023, bungeni jijini Dodoma, wakati wabunge wanapitisha mafungu ya makadirio ya mapato na matumizi ya Wizara ya Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, kwa 2023/24.
Mdee alisema atashika shilingi katika fungu namba 32 ambalo lina mshahara wa waziri wa wizara hiyo.
Mdee amedai kuwa, taarifa za Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), katika nyakati tofauti zinaonyesha malimbikizo ya madai ya watumishi yanakuwa kwa kasi, licha ya hatua inayochukuliwa na Serikali kuyalipa.
“Taarifa zimekuwa zikionyesha madai ya watumishi yamekuwa yakikuwa kwa kiwango kikubwa na madai ya waziri yamejikita kwenye mishara.
“Taarifa za CAG zimekuwa zikionyesha mfano 2020/21 madai ya watumishi yalikuwa Sh. 429 bilioni na sasa inakadiriwa kuwa Sh. 509 bilioni. Changamoto hii imekuwa kubwa kutokana na ucheleweshaji,” amesema Mdee.
Mdee amesema “tunaenda kinyume na kanuni na wacheleweshaji wakubwa ni wizara ya fedha. Nataka nipate majibu yenye tija sababu juhudi za Rais zinaonekana kupunguza lakini haziondoi. Nataka majibu, yasiporidhisha nakamata shilingi.”
Kufuatia hoja hiyo, Naibu Waziri Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Ridhiwani Kikwete, alitoa ufafanuzi akisema Rais Samia Suluhu Hassan, pamoja na Serikali yake wanaendelea kulipa malimbikizo ya madai ya watumishi.
Hata hivyo, wabunge hao walipitisha bajeti ya wizara hiyo ya Sh trilioni 1.1 ambayo iliwasilishwa bungeni jana na Simbachawene.
Duh!
Siyo ucheleweshaji. Ni wivu tu! Yaani kijana anamuonea wivu mstaafu wa miaka 60 anapotaka kuchukua haki yake ya kibunda chake! Acheni tabia hii ya wivu.
Sheria itungwe na si kulalamika tu!