Thursday , 2 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Mbowe: Miaka 62 ya uhuru tujenge upya mioyo yetu
Habari za SiasaTangulizi

Mbowe: Miaka 62 ya uhuru tujenge upya mioyo yetu

Spread the love

WAKATI Tanganyika ikiadhimisha miaka 62 tangu kupata uhuru, Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Freeman Mbowe, amewataka watanzania kuongeza jitihada za kuleta maendeleo pamoja na kukemea ubaguzi. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam…(endelea).

Mbowe ametoa wito huo leo tarehe 9 Disemba 2023, kupitia kurasa zake za mitandao ya kijamii. Tanganyika huadhimisha siku ya uhuru tarehe 9 Disemba kila mwaka.

“Tunapoadhimisha, naomba tujenge upya mioyo yetu na kuahidi kuwa jasiri tena katika harakati zetu za maendeleo na ustawi. Naomba tuwe hodari katika jitihada zetu za kujenga Tanzania inayojumuisha kila mmoja wetu bila ubaguzi, yenye haki kwa kila mmoja wetu, na yenye neema kwa wote,” ameandika Mbowe.

Mwenyekiti huyo wa Chadema amesema licha ya mafanikio mbalimbali ambayo Tanganyika imepata tangu uhuru, lakini bado inakabiliwa na janga la umasikini kwa watu wake.

“Tunaadhimisha miaka 62 ya uhuru tukikumbuka pia umasikini wa watu wetu katikati ya wingi wa rasilimali, fursa zilizopotea na ahadi zilizovunjwa kutokana na sera na uongozi ambao haukutumia nguvu na ujasiri wa Watanzania,” ameandika Mbowe.

Amewataka Watanzania waenzi juhudi za waliopigania uhuru kwa kulipigania taifa kwa ujasiri pamoja na kukataa ahadi alizoita za uongo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Chadema waendelea kulilia katiba mpya

Spread the loveCHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimeendelea kudai upatikanaji wa...

Habari za SiasaTangulizi

Chadema kumshtaki Rais Samia

Spread the loveCHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimetishia kumfungulia kesi ya...

Habari za Siasa

Tume huru ya uchaguzi yatangaza uchaguzi mdogo Jimbo la Kwahani

Spread the love  TUME Huru ya Taifa ya Uchaguzi, imetangaza uchaguzi mdogo...

AfyaHabari za Siasa

Dk. Biteko aagiza utoaji huduma saratani usiwe wa kibaguzi

Spread the loveNaibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto Biteko...

error: Content is protected !!