Friday , 3 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Mbowe atinga kortin, hukumu kutolewa leo
Habari za Siasa

Mbowe atinga kortin, hukumu kutolewa leo

Mwenyekiti wa Chadema nchini Tanzania, Freeman Mbowe (kushoto) akiwa na Wakili John Mallya katika Mahakama ya Haki ya Afrika Mashariki jijini Arusha
Spread the love

 

MAHAKAMA ya Haki ya Afrika Mashariki leo Ijumaa tarehe 25 Machi 2022 itatoa hukumu ya kesi juu ya uhalali wa Mabadiliko ya Sheria ya Vyama vya Siasa ya mwaka 2019. Anaripoti Mwandishi Wetu, Arusha … (endelea).

Kesi hiyo namba 3 ya mwaka 2020, ilifunguliwa na kiongozi wa chama kikuu cha upinzani nchini Tanzania cha Chadema, Freeman Mbowe na wenzake wakipinga mabadiliko ya sheria hiyo.

Mbowe na wenzake wanalalamikia ukiukwaji wa Mkataba wa Afrika Mashariki wa masharti ya utawala bora na haki za binadamu ambapo mabadiliko ya sheria ya vyama vya siasa yam waka 2019 inaonekana kukiukwa.

Miongoni mwa vifungu vinavyobishaniwa kwenye sheria hiyo ni pamoja na cha 5A(1) kinachozuia mtu au taasisi kutoa elimu ya uraia bila idhini ya msajili wa vyama vya siasa.

Aidha, Mbowe na wenzake wanalalamikia kifungu cha 5B(1) kinachotoa mamlaka kwa msajili kuhitaji taarifa yoyote ya chama, vifungu 6B(d),8C(2),8D(2),8E,11A(2),21(E) na 23(7).

Mbowe na wenzake wanawakilishwa na mawakili John Mallya na Jebla Kambole ambapo tayari Mbowe na Mallya wamekwisha kufika mahakamani hapo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Chadema waendelea kulilia katiba mpya

Spread the loveCHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimeendelea kudai upatikanaji wa...

Habari za SiasaTangulizi

Chadema kumshtaki Rais Samia

Spread the loveCHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimetishia kumfungulia kesi ya...

Habari za Siasa

Tume huru ya uchaguzi yatangaza uchaguzi mdogo Jimbo la Kwahani

Spread the love  TUME Huru ya Taifa ya Uchaguzi, imetangaza uchaguzi mdogo...

AfyaHabari za Siasa

Dk. Biteko aagiza utoaji huduma saratani usiwe wa kibaguzi

Spread the loveNaibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto Biteko...

error: Content is protected !!