Sunday , 5 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Mawakili wabishana Mdee wenzake kuhojiwa, uamuzi Septemba 2
Habari za Siasa

Mawakili wabishana Mdee wenzake kuhojiwa, uamuzi Septemba 2

Wakili wa Chadema, wakiongozwa na Peter Kibatala (katikati) wakiwa mahakamani
Spread the love

 

MAWAKILI wa upande wa waleta maombi wamepinga upande wa washtakiwa (Chadema), kuwahoji Halima Mdee na wenzake saba ambao waliitwa mahakamani leo kwaajili ya kuhojiwa. Anaripoti Faki Sosi na Apaikunda Mosha, Dar es Salaam … (endelea).

Mawakili hao wameweka pingamizi hilo leo Ijumaa tarehe, 26 Agosti, 2022, katika Mahakama Kuu mbele ya Jaji Cyprian Mkeha, ambapo shauri hilo liliitwa kwaajili ya kuanza kusikilizwa ambapo Mdee na wenzake wanapinga kufukuzwa uanachama wa Chadema kwa madai kuwa utaratibu ilikiukwa.

Mawakili hao wamepinga mahakama kuruhusu wateja wao kuhojiwa kwa kuwa wao ndio wanaoshitaki na kwamba upande unaotaka kuwahoji ni wa washitakiwa (Chadema).

Wakili wa washitakiwa, Peter Kibatala ameiomba Mahakama iwakumbushe amri ambazo mahakama ilitoa na Jaji Mkeha amezisoma amri hizo ikiwa ni pamoja na kuwasilishwa kwa kiapo kinzani tarehe 5 Agosti, 2022 na Mdee na wenzake kufika mahakamani tarehe 26, Agosti, 2022 saa tatu asubuhi kwaajili ya kuhojiwa.

Halima Mdee na wenzake sita wakiwa Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam

Wakili Kibatala amesema msingi wa hoja iliyotolewa ni dhaifu “mno” kisheria hazijaoana na maombi ya waleta maombi.

“Mahakama ikishatoa amri mikono ya mahakama imefungwa, wenzetu wameshathibitisha walioitwa na mahakama wapo, mahakama itekeleze amri yake,” amesema Kibatala.

Edson Kilatu wakili wa kina Mdee amedai kuwa pingamizi la awali linaweza kuwasilishwa na upande wowote katika shauri, “sio kama anavyodai Wakili Peter Kibatala kuwa ni silaha ya wajibu maombi.”

Jaji Mkeha amesema kuwa atatoa uamuzi tarehe 2 Septemba 2022 saa nane na nusu mchana na kuwataka Mdee na wenzake saba waliotakiwa kuhojiwa leo wasiende mahakamani mpaka mahakama hiyo itakapotoa uamuzi wa pingamizi hilo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Mbatia ambwaga Selasini, mahakama yaamuru alipwe fidia

Spread the loveMAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Kisutu, jijini Dar es Salaam, imemuamuru...

Habari za SiasaTangulizi

Mkulo afariki dunia, kuzikwa kesho Kilosa

Spread the loveALIYEKUWA Waziri wa Fedha na Mbunge wa Kilosa (CCM), Mustafa...

Habari za SiasaTangulizi

Sabaya afutiwa kesi, ruksa kugombea uongozi

Spread the loveMwendesha Mashtaka Mkuu wa Serikali DPP leo Ijumaa amefuta rufaa...

Habari za Siasa

Serikali yasaka bilioni 3 kujenga daraja Mto Mpiji

Spread the loveSerikali imesema inaendelea na juhudi za kutafuta fedha kiasi cha...

error: Content is protected !!