Friday , 26 April 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa Marekani yapiga marufuku uagizaji mafuta kutoka Urusi
Kimataifa

Marekani yapiga marufuku uagizaji mafuta kutoka Urusi

Spread the love

 

RAIS wa Marekani, Joe Biden ametangaza kuwa nchi hiyo yake imepiga marufuku ununuzi wa gesi, mafuta na makaa ya mawe kutoka Urusi. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Jana tarehe 8 Machi, 2022 Rais Biden ametangaza marufuku hiyo ya kuagiza bidhaa za mafuta na nishati kutoka Urusi kama njia mojawapo ya kuiadhibu nchi hiyo iliyoamua kuivamia kivita taifa la Ukraine.

“Tunapiga marufuku uagizaji wa bidhaa zote za mafuta na gesi kutoka Urusi. Hatua hiyo inamaanisha kuwa bidhaa zote za nishati hazitakubaliwa kusafirishwa katika bandari ya Marekani,” Rais Biden aliwaambia waandishi wa habari Ikulu ya White House.

Wakati hayo yakijiri taifa la Uingereza limesema kwamba litapiga marufuku ununuzi wa mafuta hayo pamoja na bidhaa nyinginezo za nishati mwishoni mwa mwaka huu.

Aidha, limewaruhusu wafanyabiashara na wasambazaji wa bidhaa hiyo kwa muda huku wakiendelea kutafuta njia mbadala.

Naye Waziri wa Mambo ya Nje wa Ujerumani, Annalena Baerbock amenukuliwa na Shirika la habari la Ufaransa (AFP) akisema kuwa, nchi yake inapinga vikwazo vya kutoagiza bidhaa za nishati kutoka Urusi.

Baerbock amesema iwapo Ujerumani itazuia kuingiza nchini humo kwa bidhaa hizo kutoka Urusi, umeme utakatika nchini humo hivyo watalazimika kuviondoa vikwazo hivyo wao wenyewe ili uchumi wake usisambaratike.

Taifa la Ujerumani linategemea kwa asilimia 55 gesi na asilimia 42 ya mafuta na makaa ya mawe vyote kutoka Urusi.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

KimataifaTangulizi

Mkuu wa majeshi Kenya afariki, Ruto atangaza maombolezo

Spread the loveRais wa Kenya, William Ruto ametangaza maombezo ya siku tatu...

Kimataifa

Majaji kuamua hatima ya Zuma leo

Spread the loveMajaji nchini Afrika Kusini leo Jumanne wataamua ikiwa rais wa...

Habari za SiasaKimataifa

Spika Afrika Kusini ajiuzulu kwa tuhuma za rushwa

Spread the loveSpika wa Bunge la Afrika Kusini, Nosiviwe Mapisa-Nqakula ametangaza kujiuzulu...

Habari MchanganyikoKimataifa

Tetemeko la ardhi laua 7, lajeruhi 800 Taiwan

Spread the loveWatu wapatao saba wamefariki dunia na wengine zaidi ya 800...

error: Content is protected !!