Friday , 3 May 2024
Home Kitengo Michezo Manara amaliza utata
Michezo

Manara amaliza utata

Haji Manara
Spread the love

MSEMAJI wa klabu ya Simba, Haji Manara amesema kuwa bado yupo sana ndani ya klabu ya Simba na wala hana mpango wa kuondoka katika siku za hivi karibuni kama taarifa za hapo awali zilivyokuwa zinaeleza. Anaripoti Kelvin Mwaipungu, Dar es Salaam … (endelea).

Siku za hivi karibuni Manara alisema kuwa mara anampango wa kuuomba uongozi wa klabu hiyo kupumzika katika nafasi yake ya Mkuu wa kitengo cha Habari ndani ya timu hiyo kutokana na kuteteleka kwa afya yake.

Manara ametoa kauli hiyo leo wakati wa Tamasha la Simba Day lililofanyika kwenye Uwanja wa Benjamini Mkapa, Jijini Dar es Salaam ambapo aliwaambia mashabiki wa klabu hiyo kuwa wafute mawazo ya yeye kuondoka ndani ya klabu hiyo.

“Niwaambie kitu mashabiki wa Simba, mimi bado nipo nipo sana ndani ya Simba na wala sina mpango wa kuondoka leo wala kesho, naombeni mfute hayo mawazo,” alisema Haji.

Manara ameyaeleza hayo wakati alipomaliza kuwatambulisha wachezaji watakao tumika na klabu hiyo katika msimu ujao wa mashindano huku kukiwa na maingizo mapya saba.

Msemaji huyo ambaye leo alishuka uwanjani hapo na helkopta akiwa sambamba na Msanii wa mziki wa kizazi kipya, Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’ ambaye alitumbuiza kwenye tamasha hilo.

1 Comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Michezo

Europa na Conference kukupatia pesa ndefu leo

Spread the love  ALHAMISI ya leo tutaenda kushuhudia mitanange ya kukata na...

Habari MchanganyikoMichezo

Wanamichezo Mei Mosi wachangia wahitaji vitu vya mil. 11.5

Spread the loveWanamichezo wanaoshiriki Michezo ya Mei Mosi Taifa 2024 jijini Arusha...

Michezo

Usiku wa Ulaya umerejea kibabe kabisa

Spread the love  LIGI ya Mabingwa barani Ulaya imerejea tena na awamu...

Habari MchanganyikoMichezo

Mambo ya Ndani, Ulinzi zang’ara michezo ya Mei Mosi Arusha

Spread the loveRais wa Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi nchini (TUCTA), Tumaini...

error: Content is protected !!