KANISA la Kiinjili la Kilutheri Tanzania limeonya watu kuacha tabia ya kujilimbikizia mali na kula rushwa kwa kuwa matendo hayo yamepigwa vita na Mungu. Anaripoti Faki Sosi…(endelea)
Akihutubia katika Misa takatifu ya kuadhimisha kuzaliwa kwa Yesu Kristo leo tarehe 25 Desemba 2023 katika Kanisa la KKKT Azania Front jijini Dar es Salaam Askofu Mkuu wa Kanisa hilo Alex Malasusa amewataka wakristo na Watanzania kuacha ubaya na tamaa za kidunia ikiwa pamoja na kula rushwa.
“Dunia imejaa ubaya na tamaa watu wamejaa tamaa katika dunia hii unapozungumzia rushwa na nimesikitika kusikia kwamba rushwa inaanza tena kukua kwa sababu rushwa ni roho yakutokuridhika, rushwa, dhulma na mambo mengine mengi yanayofanywa.”
“Paul anasema tuukatae ubaya na tamaa za dunia sasa tuamue kuishi kwa kiasi, ni kuishi kwa kuridhika”.
Amesema kuwa maandiko yapo wazi kuwa yanafundisha watu kutosheka.
“Nilikuwa najiuliza kwanini katika Sala ile Bwana Yesu aliyotufundifa ‘Tupe leo riziki yetu tafsiri yake kamili utupe leo mkate wetu wa kila siku nikajiuliza kwanini hakutuambia utupe mikate yetu mpaka tutakapokufa kuna watu wanamikate mpaka ya vitukuu yaani anajaza hatosheki tunaambiwa tuishi kwa kiasi ” Amesema Malasusa.
Amesema kuwa hulka ya watu wasiotosheka ni kuwadhulumu wengine waliostahili na kwamba kama dunia ingekuwa ya haki tusengekuwa na masikini kiasi hiki lakini pia kama dunia ingekuwa na watu wenye huruma ingekuwa sehemu watu wanapopenda.
“Ukisikia mtu yoyote amekatisha uhai wake jiulize mchango wako ni nini wako watu wanakufa kwa sababu ya kukosa matibabu jiuze kwa sababu gani,” amehoji.
Leave a comment