Friday , 3 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Maimamu Tz waipongeza Afrika Kusini kwa kuishtaki Israel ICJ
Habari za Siasa

Maimamu Tz waipongeza Afrika Kusini kwa kuishtaki Israel ICJ

Spread the love

SHURA ya Maimamu Tanzania, imewasilisha pongezi zake kwa Serikali ya Afrika Kusini, kufuatia uamuzi wake wa kuishtaki Israel katika Mahakama ya Kimataifa ya Haki (ICJ), ikiituhumu kwa mauaji ya halaiki katika vita inayoendelea ukanda wa Gaza dhidi yake na kundi la wanamgambo wa Kipalestina la Hamas. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam…(endelea).

Pongezi hizo ziliwasilishwa na viongozi hao wa kiislamu katika Ubalozi wa Afrika Kusini nchini Tanzania, tarehe 24 Januari mwaka huu.

Katibu Mkuu wa Shura ya Maimamu, Sheikh Ponda Issa Ponda, amesema “Tumepeleka salamu kwa Balozi wa Afrika Kusini, sehemu ya waraka wetu inasema ingawa hukumu ya mahakama ya kimataifa haijatoka lakini tayari mmeshinda katika mahakama ya ubinadamu na mahakama ya maoni ya watu. Kitendo chenu kimegusa nyoyo na akili za mamilioni ya watu duniani.”

Kupitia waraka huo wa Shura ya Maimamu kwenda kwa Afrika Kusini, wamesema uamuzi wao huo umerejesha imani kuwa ubinadamu haujafa na kuchochea ari ya kupigania haki za Wapalestina.

Mapigano kati ya Hamas na Israel yaliibuka Oktoba 2023 baada ya wanamgambo wa kundi hilo kufanya mashambulizi ya kushtukiza yaliyosababisha mauaji ya maelfu ya watu wengi wao wakiwa waisrael.

Baada ya shambulizi hilo, Israel ilijibu mapigo kitendo kilichoibua muendelezo wa vita iliyopoteza maisha ya maelfu ya watu.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Chadema waendelea kulilia katiba mpya

Spread the loveCHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimeendelea kudai upatikanaji wa...

Habari za SiasaTangulizi

Chadema kumshtaki Rais Samia

Spread the loveCHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimetishia kumfungulia kesi ya...

Habari za Siasa

Tume huru ya uchaguzi yatangaza uchaguzi mdogo Jimbo la Kwahani

Spread the love  TUME Huru ya Taifa ya Uchaguzi, imetangaza uchaguzi mdogo...

AfyaHabari za Siasa

Dk. Biteko aagiza utoaji huduma saratani usiwe wa kibaguzi

Spread the loveNaibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto Biteko...

error: Content is protected !!