Friday , 3 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Mahakama yakubali kusikiliza mapingamizi ya akina Mdee
Habari za SiasaTangulizi

Mahakama yakubali kusikiliza mapingamizi ya akina Mdee

Spread the love

MAHAKAMA Kuu Kanda ya Dar es Salaam imeamua kusikiliza mapingamizi yaliyowasilishwa mahakamani hapo na Mawakili wa Mbunge wa viti Maalum (Chadema), Halima Mdee na wenzake 18 kabla ya kuendelea na usikilizwaji wa shauri hilo. Anaripoti Faki Ubwa… (endelea)

Jaji Cyprian Mkeha alitoa uamuzi huo jana tarehe 2 Septamba 2022, kutokana na majibizano ya hoja za mawakili wa upande waombaji kina mdee na zile za wajibu maombi namba moja (Chadema).

Kwenye shauri hilo namba 36 la mwaka 2022 Mdee na wenzake wanawashtaki Chadema, Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) na Mwanasheria Mkuu wa Serikali (A. G).

Upande huo unawakilishwa na Ipilinga Panya, Edson Kilatu, Emmanuele Uhashu, na Aliko Mwananenge. Huku  Stanley Kaloka akiongoza jopo la Mawakili wa Serikali kwa ajili ya mjibu maomba namba mbili NEC na namba tatu AG.

Upande wa wajibu maombi namba moja (Chadema) uliongozwa na Wakili Peter Kibatala, Jeremiah Mtobesya, Omary Msemo, Dickson Matata, Suleiman Makauka, Deogratius Mahenyela.

Awali tarehe 26 Agosti shauri hilo lilipangwa kwa ajili ya usikilizwaji ambapo Mahakama ilitoa amri ya kufika kwa Mdee na wenzake saba kwa ajili ya kuhojiwa na upande wa mawakili wa Chadema.

Mdee na wenzake walifika lakini mawakili wao waliibuka na hoja ya kupinga kuhojiwa na kuendelea na usikilizwaji kwa kupinga kiapo kinzani cha upande wa wajibu maombi namba moja (Chadema) kwa kudai kuwa kinakasoro zitakazoathiri mwenendo wa shauri hilo.

Jana Jaji Mkeha alipokuwa anatoa uamuzi wake alisema atasikiliza pingamizi hilo kwa kuwa utaratibu unaolekeza kuwa huwezi kuendelea kusikiliza shauri kukiwa kuna mapingamizi.

Alisema kuwa wakati shauri hilo linaanza, mawakili wa pande zote walikuwa wanakiu ya shauri hilo lisikilizwe mapema na kuahidi kutokuweka mapingamizi yatakayokwamisha usikilizwaji wake.

Jaji Mkeha aliendelea kuwakumbusha mawakili ahadi yao hiyo huku akisema kuwa tarehe 26 Agosti, 2022 upande wa waombaji ulikwenda kinyume na ahadi yao kwa kuweka pingamizi la kutoendelea kusikilizwa kwa shauri hilo mpaka lisikilizwe pingamizi hilo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Chadema waendelea kulilia katiba mpya

Spread the loveCHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimeendelea kudai upatikanaji wa...

Habari za SiasaTangulizi

Chadema kumshtaki Rais Samia

Spread the loveCHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimetishia kumfungulia kesi ya...

Habari za Siasa

Tume huru ya uchaguzi yatangaza uchaguzi mdogo Jimbo la Kwahani

Spread the love  TUME Huru ya Taifa ya Uchaguzi, imetangaza uchaguzi mdogo...

AfyaHabari za Siasa

Dk. Biteko aagiza utoaji huduma saratani usiwe wa kibaguzi

Spread the loveNaibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto Biteko...

error: Content is protected !!