Friday , 3 May 2024
Home Habari Mchanganyiko Mafuriko yaua 33 Morogoro, Pwani
Habari MchanganyikoTangulizi

Mafuriko yaua 33 Morogoro, Pwani

Spread the love

 

SERIKALI ya Tanzania imetoa tathmini ya athari ya mafuriko yanayosababishwa na mvua kubwa inayonyesha mfululizo katika baadhi ya mikoa nchini, ikisema yameua watu 28 mkoani Morogoro na watano Pwani. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam…(endelea).

Ripoti ya athari ya mafuriko imetolewa leo Ijumaa, tarehe 12 Aprili 2024, jijini Dar es Salaam na Msemaji Mkuu wa Serikali, Mobhare Matinyi, huku Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA), ikitoa tahadhari ya uwepo wa mvua kubwa katika mikoa ya Dar es salaam, Tanga, Morogoro, Pwani, Lindi na Mtwara, kati ya tarehe 12 hadi 14 Aprili mwaka huu.

Matinyi amesema mafuriko hayo pamoja na kusababisha vifo, imeleta maafa katika halmashauri nane za Morogoro ambapo nyumba zaidi ya 6,800 zikizingirwa maji na kubomoa 1,035.

“Morogoro kuna vifo 28 na Pwani kuna vifo vya watu watano, watu wawili wamefariki wilayani Rufiji na wawili Kibiti na mmoja Kisarawe. Majeruhi wawili wilayani Kibiti na majeruhi watatu Kisarawe. Makazi ya barabara, makazi, madaraja nguzo ya umeme, shule na kituo cha afya mhoro Rufiji kimesomwa na maji, lakini kuna uharibifu wa mazao mengi ya chakula mahindi, mpunga, ufuta, ndizi mihogo na mtama,” amesema Matinyi.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Chadema waendelea kulilia katiba mpya

Spread the loveCHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimeendelea kudai upatikanaji wa...

Habari za SiasaTangulizi

Chadema kumshtaki Rais Samia

Spread the loveCHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimetishia kumfungulia kesi ya...

BiasharaHabari Mchanganyiko

NMB yang’ara maonesho OSHA

Spread the loveBenki ya NMB imebeba tuzo ya kampuni bora kwenye sekta...

Habari MchanganyikoKimataifa

Ruto amteua Kahariri kuwa mkuu wa majeshi

Spread the loveRAIS wa Kenya, William Ruto, amemteua Jenerali Charles Muriu Kahariri,...

error: Content is protected !!