MAASKOFU wa Kanisa Katoliki nchini Tanzania, Paul Ruzoka wa Jimbo Kuu la Tabora na Severin Niwemugizi wa Jimbo la Rulenge-Ngara mkoani Kagera, wamepata ajali gari eneo la Buziku, wilayani Chato mkoa wa Geita. Anaripoti Mwandishi Wetu, Chato … (endelea).
Ajali hiyo imetokea mchana wa leo Alhamisi, tarehe 4 Novemba 2021, wakati maaskofu hao wakitoka kikaoni Mwanza, kwenga Ngara katika msiba wa Padre wa Jimbo hilo aliyefariki dunia jana Jumatano.
Akizungumza na MwanaHALISI Online kwa simu, Askofu wa Jimbo la Geita, Fravian amesema, maaskofu hao walikuwa katika kikao cha kamati tendaji cha Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania (TEC), Igombe jijini Mwanza.
Amesema, jana Jumatano kuna Padre wa Jimbo la Rulenge-Ngara alifariki dunia katika Hospitali ya Bugando, Mwanza hivyo kulazimka kwenda msibani na Askofu Ruzoka akamsindikiza.
“Ni kweli ajali imetokea kabla ya saa 6 mchana, baada ya kutokea kwa msiba wa Padre wa Jimbo hilo, wameondoka asubuhi na wakiwa wamepita eneo la Buziku kuna mtu aliingia barabarani ghafla.
“Katika jitihada za kumkwepa yule mtu akarudi ule upande waliokuwa wamemkwepea, ili wasimdhulu ikabidi amkwepe tena upande wa pili na ndipo gari ilipoanguka,” amesema Askofu Kasala
Amesema “kwa bahati yule mtu hakudhulika na maaskofu wametoka salama na wameumia kidogo.”
Askofu Kasala amesema, “baada ya ajali hiyo wamepelekwa Parokoa ya Buziku na baadaye wamepelekwa Hospitali ya Biharamulo kwa ajili ya uchunguzi ili kuona hali zao kabla ya kuendelea na safari.”
Leave a comment