Sunday , 28 April 2024
Home Kitengo Maisha Afya Kipindupindu chasababisha shule kutofunguliwa Zambia
AfyaKimataifa

Kipindupindu chasababisha shule kutofunguliwa Zambia

Spread the love

Serikali ya Zambia imetangaza kuahirisha kuanza kwa muhula mpya ya masomo kwa wiki tatu zaidi kutokana mlipuko wa ugonjwa wa kipindupindu ambao umeshaua watu 150 tangu Oktoba, 2023. Inaripoti Mitandao ya Kimataifa …(endelea).

Waziri wa Elimu nchini humo, Douglas Syakalima amesema shule nchini humo zilipaswa kufunguliwa tarehe 8 Januari 2024 lakini sasa zitafunguliwa tarehe 29 Januari  2024.

Zaidi ya watu 4,000 wameugua kipindupindu na vifo 150 vimeripotiwa, takwimu za hivi karibuni za Serikali zinaonyesha kiwango cha vifo ni asilimia 3.7.

“Serikali ina wasiwasi kuhusu athari za mlipuko wa ugonjwa wa kipindupindu katika sekta ya elimu, hivyo hatua hiyo imechukuliwa ili kulinda afya za wanafunzi,” amesema Syakalima.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaKimataifaTangulizi

Tanzania, Somalia kuibua maeneo mapya ya ushirikiano

Spread the love  RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amesema Tanzania na Somalia...

Afya

Mloganzila yajipanga kupandikizaji wa ini

Spread the love  HOSPITALI ya Taifa Muhimbili-Mloganzila imesema kutokana na uwekezaji uliofanywa...

KimataifaTangulizi

Mkuu wa majeshi Kenya afariki, Ruto atangaza maombolezo

Spread the loveRais wa Kenya, William Ruto ametangaza maombezo ya siku tatu...

Kimataifa

Majaji kuamua hatima ya Zuma leo

Spread the loveMajaji nchini Afrika Kusini leo Jumanne wataamua ikiwa rais wa...

error: Content is protected !!