Friday , 3 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Kinana atangaza ziara mikoa 11
Habari za SiasaTangulizi

Kinana atangaza ziara mikoa 11

Abdulrahman Kinana, Makamu Mwenyekiti wa CCM Bara
Spread the love

 

MAKAMU Mwenyekiti wa chama tawala nchini Tanzania- Chama Cha Mapinduzi (CCM)-Bara, Abdulrahman Kinana ametangaza ziara ya kichama ya mikoa minne atakayoifanya hivi karibuni. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).

Kinana ametangaza ziara hiyo leo Jumapili, tarehe 10 Aprili 2022, katika ukumbi wa Diamond Jubelee wakati CCM Mkoa wa Dar es Salaam walipomwandalia mapokezi rasmi, baada ya kuchaguliwa kwenye nafasi hiyo.

Alichaguliwa na mkutanomkuu maalum tarehe 1 Aprili 2022 jijini Dodoma, akichukua nafasi ya Philip Mangula aliyetangaza kung’atuka, mara baada ya kukitumikia chama hicho kwa nafasi mbalimbali kwa kipindi kirefu.

Kinana aliyewahi kuwa katibu mkuu wa chama hicho amesema, mara baada ya kuingia ofisini na kuzoea mazingira na majukumu yake, “nitafanya ziara katika mikoa ya Pwani, Tanga, Kilimanjaro na Arusha.”

“Baada ya kumaliza mikoa hii minne, nitaanza ziara ya mikoa mingine saba kwa mpigo. Lazima chama chetu kiwe imara na tusipokuwa na chama imara kama alivyosema Mwalimu Nyerere Taifa letu litayumba.”

Hata hivyo, Kinana hakubainisha mikoa hiyo mingine saba kwa majinga ingawa amesema, wakati ukifika atajulisha.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Chadema waendelea kulilia katiba mpya

Spread the loveCHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimeendelea kudai upatikanaji wa...

Habari za SiasaTangulizi

Chadema kumshtaki Rais Samia

Spread the loveCHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimetishia kumfungulia kesi ya...

Habari za Siasa

Tume huru ya uchaguzi yatangaza uchaguzi mdogo Jimbo la Kwahani

Spread the love  TUME Huru ya Taifa ya Uchaguzi, imetangaza uchaguzi mdogo...

AfyaHabari za Siasa

Dk. Biteko aagiza utoaji huduma saratani usiwe wa kibaguzi

Spread the loveNaibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto Biteko...

error: Content is protected !!