Tuesday , 7 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Kigogo CCM: Hatuwezi kushinda uchaguzi kwa mabavu
Habari za Siasa

Kigogo CCM: Hatuwezi kushinda uchaguzi kwa mabavu

Issa Gavu
Spread the love

KATIBU wa Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC) ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) Idara ya Oganaizesheni, Issa Gavu, amesema chama hicho hakiwezi kushinda kwa kutumia njia za mabavu katika chaguzi, bali ili kishinde kinatakiwa kuandaa wagombea bora pamoja na kuhamasisha wananchi washiriki zoezi hilo. Anaripoti Mwandishi Wetu, Shinyanga…(endelea).

Gavu ametoa kauli hiyo jana Jumanne, akizungumza na baadhi ya viongozi wa CCM mkoani Shinyanga.

Katibu huyo wa organaizesheni CCM, alisema chama hicho kinapaswa kuandaa utaratibu wa kuwa na viongozi wawajibikaji, wanaojituma na kufanya kazi, ili waweze kuaminiwa na wananchi.

“Tunakwenda mwaka kesho utakuwa mwaka wa uchaguzi, njia pekee ya kuhakikisha kwamba chama chetu kinashinda ni kutengeneza utaratibu mzuri wa kuwa na viongozi wawajibikaji, wanaoweza kujituma na kufanya kazi. Hatuwezi kushinda kwenye mfumo wa vyama vingi kwa kutumia njia za mabavu,” alisema Gavu na kuongeza:

“Ili muende vizuri utakapofika wakati wa uboreshaji daftari la wapiga kura tuhakikishe tunahamasisha wanachama na wananchi wetu wajitokeze kwa wingi wakajiandikishe katia daftari ili ukifika wakati chama chetu kiwe na watu wengi waliojiandikisha ili mwisho wa siku kura zetu ziwe nyingi kuliko vyama vingine.”

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Jacob, Malisa wapandishwa kizimbani kwa mashtaka ya uongo mitandaoni

Spread the loveMKURUGENZI wa Shirika la Haki, Godlisten Malisa na mwanachama wa...

BiasharaHabari za Siasa

Bunge laitaka Serikali kudhibiti ufisadi miradi ya mkakati

Spread the loveKAMATI ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu, imeitaka Serikali kuimarisha...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Wizara ya Uchukuzi yaomba kuongezewa bajeti na Bunge

Spread the loveWIZARA ya Uchukuzi imeliomba Bunge liidhinishe bajeti yake kwa mwaka...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Serikali kutafuta mwekezaji mwingine Bandari ya Dar es Salaam

Spread the loveSERIKALI inaendelea kutafuta mwekezaji mwingine atakayeendesha gati namba nane hadi...

error: Content is protected !!