Friday , 3 May 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa Israel, Hamas kusitisha mapigano kwa muda
Kimataifa

Israel, Hamas kusitisha mapigano kwa muda

Spread the love

NCHI ya Israel, pamoja na kikundi cha wanamgambo wa kiislamu, Hamas, wamekubaliana kusitisha mapigano katika Ukanda wa Gaza, ili kuruhusu zoezi la kuacha huru mateka wa pande zote mbili. Inaripoti Mtandao ya Kimataifa…(endelea).

Kwa mujibu wa mtandao wa BBC Swahili, uamuzi huo wa kusitishwa kwa mapigano kwa muda wa siku nne mfululizo ili kutoa nafasi ya mateka wa pande zote mbili kuachwa huru, unafuatia hatua ya Serikali ya Israel kuidhinisha mpango wa kuwaacha huru mateka wa Palestina zaidi ya 150, wakiwemo wanawake na watoto.

Kwa upande wa Hamas, umetoa taarifa iliyodai kwamba, endapo wapalestina 150 wataachwa huru kutoka katika jela za Israel, chini ya makubaliano maalum, watawaachia mateka wa Israel 50.

Mbali na kubadilishana mateka, makubaliano hayo yametajwa kuruhusu uingizaji wa malori yanayobeba misaada ya kibinadamu, vifaa vya matibabu na mafuta, kuingia upande wa Gaza.

Uamuzi wa kuachwa huru mateka, unajiri baada ya Shirika linalotetea haki za binadamu, Human Right Watch, kudai takribani wapalestina 7,000 wakiwemo wanawake na watoto wanazuiliwa katika magereza ya Israel, huku wakihojiwa bila kupata uwakilishi wa kisheria.

Kwa sasa mitandao ya kimataifa imeripoti kuwa, majeshi ya Israel yanaendelea kuishambulia Gaza.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaKimataifa

Mwanamke Rwanda ataka kupambana tena na Kagame

Spread the loveKIONGOZI wa kihistoria wa upinzani nchini Rwanda, Victoire Ingabire Umuhoza,...

Habari MchanganyikoKimataifa

Ruto amteua Kahariri kuwa mkuu wa majeshi

Spread the loveRAIS wa Kenya, William Ruto, amemteua Jenerali Charles Muriu Kahariri,...

Habari za SiasaKimataifaTangulizi

Tanzania, Somalia kuibua maeneo mapya ya ushirikiano

Spread the love  RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amesema Tanzania na Somalia...

KimataifaTangulizi

Mkuu wa majeshi Kenya afariki, Ruto atangaza maombolezo

Spread the loveRais wa Kenya, William Ruto ametangaza maombezo ya siku tatu...

error: Content is protected !!