Tuesday , 21 March 2023
Home Gazeti Habari Mchanganyiko Hii hapa kauli ya Sheikh mpya mkoa wa Dar
Habari MchanganyikoTangulizi

Hii hapa kauli ya Sheikh mpya mkoa wa Dar

Spread the love

SAA chache baada ya kuteuliwa kukaimu nafasi ya aliyekuwa Sheikh wa mkoa wa Dar es Salaam, Alhad Mussa Salum, Sheikh mpya wa mkoa huo Sheikh Walid Alhad Omar amesema ameupokea uteuzi huo na kuahidi kumsaidia Mufti Mkuu wa Tanzania, Abubakar Zubeir. Anaripoti Mwandishi Wetu …(endelea).

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es salaam leo tarehe 2 Februari 2023, Sheikh omar amesema anamuomba Mwenyezi Mungu amsaidie kutekeleza majukumu kutokana na uteuzi huo.

“Nimepokea uteuzi wa Mufti Mkuu wa Tanzania, Abubakar Zubeir…namuomba Mwenyezi Mungu anisaidie kutekeleza uteuzi huu uliokuja, lakini kama inavyojulikana lengo la uteuzi ni kumsaidia katika yale aliyopanga kusaidia jamii ya waislamu wa Tanzania na umma wote kwa ujumla.

“Namuomba Mwenyezi Mungu aniwezeshe kwa fadhila zake kukaimu nafasi hiyo,” amesema Sheikh Omar.

Awali Katibu wa Baraza la Ulamaa, Sheikh Hassan Said Chizenga alitangza Baraza la Ulamaa la Bakwata katika kikao kilichofanyika tarehe 1 Februari 2023 chini Mwenyekiti Mufti Abubakar Zubeir limetengeua uteuzi wa Sheikh Alhad Mussa Salum kama Sheikh wa mkoa Dar es Salaam kuanzia leo tarehe 2 Februari 2023.

Sheikh Chizenga amesema baraza hilo limemteua  Sheikh Walid Alhad Omar kukaimu nafasi hiyo ya Sheikh Alhad Mussa Salum kuanzia leo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Tanzania yakabidhi rasmi msaada nchini Malawi

Spread the loveWAZIRI wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki,...

Habari Mchanganyiko

Bashe: Tumeshagawa pikipiki 5,500 kati ya 7,000 kwa maafisa ugani

Spread the love  WAZIRI wa Kilimo, Hussen Bashe, amesema wizara hiyo tayari...

Habari Mchanganyiko

Spika Tulia awapa neno mawaziri utekelezaji mashamba ya pamoja

Spread the love  SPIKA wa Bunge, Dk. Tulia Ackson, amewataka mawaziri kushirikiana...

Habari Mchanganyiko

Ukosefu wa maadili kwa wakunga, wauguzi bado changamoto

Spread the loveIMEELEZWA kuwa vitendo vya uvunjifu wa maadili kwa  wauguzi na...

error: Content is protected !!