Friday , 3 May 2024
Home Habari Mchanganyiko Hii hapa kauli ya Sheikh mpya mkoa wa Dar
Habari MchanganyikoTangulizi

Hii hapa kauli ya Sheikh mpya mkoa wa Dar

Spread the love

SAA chache baada ya kuteuliwa kukaimu nafasi ya aliyekuwa Sheikh wa mkoa wa Dar es Salaam, Alhad Mussa Salum, Sheikh mpya wa mkoa huo Sheikh Walid Alhad Omar amesema ameupokea uteuzi huo na kuahidi kumsaidia Mufti Mkuu wa Tanzania, Abubakar Zubeir. Anaripoti Mwandishi Wetu …(endelea).

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es salaam leo tarehe 2 Februari 2023, Sheikh omar amesema anamuomba Mwenyezi Mungu amsaidie kutekeleza majukumu kutokana na uteuzi huo.

“Nimepokea uteuzi wa Mufti Mkuu wa Tanzania, Abubakar Zubeir…namuomba Mwenyezi Mungu anisaidie kutekeleza uteuzi huu uliokuja, lakini kama inavyojulikana lengo la uteuzi ni kumsaidia katika yale aliyopanga kusaidia jamii ya waislamu wa Tanzania na umma wote kwa ujumla.

“Namuomba Mwenyezi Mungu aniwezeshe kwa fadhila zake kukaimu nafasi hiyo,” amesema Sheikh Omar.

Awali Katibu wa Baraza la Ulamaa, Sheikh Hassan Said Chizenga alitangza Baraza la Ulamaa la Bakwata katika kikao kilichofanyika tarehe 1 Februari 2023 chini Mwenyekiti Mufti Abubakar Zubeir limetengeua uteuzi wa Sheikh Alhad Mussa Salum kama Sheikh wa mkoa Dar es Salaam kuanzia leo tarehe 2 Februari 2023.

Sheikh Chizenga amesema baraza hilo limemteua  Sheikh Walid Alhad Omar kukaimu nafasi hiyo ya Sheikh Alhad Mussa Salum kuanzia leo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Chadema waendelea kulilia katiba mpya

Spread the loveCHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimeendelea kudai upatikanaji wa...

Habari za SiasaTangulizi

Chadema kumshtaki Rais Samia

Spread the loveCHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimetishia kumfungulia kesi ya...

BiasharaHabari Mchanganyiko

NMB yang’ara maonesho OSHA

Spread the loveBenki ya NMB imebeba tuzo ya kampuni bora kwenye sekta...

Habari MchanganyikoKimataifa

Ruto amteua Kahariri kuwa mkuu wa majeshi

Spread the loveRAIS wa Kenya, William Ruto, amemteua Jenerali Charles Muriu Kahariri,...

error: Content is protected !!