Friday , 3 May 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa Harusi yageuka msiba 100 wakifariki kwa ajali ya moto
Kimataifa

Harusi yageuka msiba 100 wakifariki kwa ajali ya moto

Spread the love

 

WATU takribani 100, akiwemo bibi na bwana harusi, wamefariki dunia kwa ajali ya moto iliyotokea usiku wa jana Jumanne, katika ukumbi waliokuwa wanafanya sherehe, ulioko kwenye Wilaya ya al-Hamdaniyah, nchini Iraq. Inaripoti Mitandao ya Kimataifa … (endelea).

Kwa mujibu wa mtandao wa BBC Swahili, takwimu hizo zimetolewa na Naibu Mkuu wa Kurugenzi ya Afya ya Ninawi, Ahmed Dubardani, akizungumza na waandishi wa habari kuhusu tukio hilo.

Dubardani alisema watu wengine 150 wamejeruhiwa katika ajali hiyo ya moto, ambapo 50 hali zao kiafya ni tete baada ya kuungua sehemu kubwa ya mwili huku wanaendelea kupatiwa matibabu hospitalini.

Mtandao wa Aljazeera nao umeripoti kuwa, maafa hayo yametokea baada ya jengo kubomoka kufuatia ajali hiyo ya moto.

Hadi sasa mamlaka nchini humo zimetoa wito kwa wananchi kuchangia damu kwa ajili ya kusaidia majeruhi.

Mazishi ya watu waliofariki katika ajali hiyo yanatarajiwa kufanyika mchana wa leo Jumatano.

Kufuatia tukio hilo, Waziri Mkuu wa Iraq, Mohammed Shia al-Sudani, ametangaza siku tatu za maombelezo.

Hadi sasa mamlaka nchini Iraq hazijaeleza chanzo cha moto huo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaKimataifa

Mwanamke Rwanda ataka kupambana tena na Kagame

Spread the loveKIONGOZI wa kihistoria wa upinzani nchini Rwanda, Victoire Ingabire Umuhoza,...

Habari MchanganyikoKimataifa

Ruto amteua Kahariri kuwa mkuu wa majeshi

Spread the loveRAIS wa Kenya, William Ruto, amemteua Jenerali Charles Muriu Kahariri,...

Habari za SiasaKimataifaTangulizi

Tanzania, Somalia kuibua maeneo mapya ya ushirikiano

Spread the love  RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amesema Tanzania na Somalia...

KimataifaTangulizi

Mkuu wa majeshi Kenya afariki, Ruto atangaza maombolezo

Spread the loveRais wa Kenya, William Ruto ametangaza maombezo ya siku tatu...

error: Content is protected !!