Friday , 26 April 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa Gavana Benki Kuu ajitosa urais
Kimataifa

Gavana Benki Kuu ajitosa urais

Gavana wa Benki Kuu ya Nigeria (CBN), Godwin Emefiele
Spread the love

 

GAVANA wa Benki Kuu ya Nigeria (CBN), Godwin Emefiele amejitosa katika kinyang’anyiro cha kuteuliwa na chama cha All Progressive Congress kuwa mgombea urais kwenye uchaguzi mkuu unaotarajiwa kufanyika mwaka kesho. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Msemaji wa chama hicho, Joseph Morka amewaeleza waandishi wa habari kuwa gavana huyo mwenye umri wa miaka 60, amechukua fomu kwa thamani ya zaidi ya Sh milioni 500 kuwania kumrithi Rais wa sasa Muhammadu Buhari ambaye anamaliza muda wake.

Gavana huyo amehudumu katika nafasi hiyo nyeti kwenye sekta ya fedha tangu mwaka 2014, baada ya kuteuliwa na Rais wa Nigeria wakati huo, Goodluck Jonathan kisha Buhari.

Kufuatia uamuzi huo, sasa Gavana huyo amekumbana na shinikizo la kutakiwa kujiuzulu kutokana na sheria za nchi hiyo kumtaka mtumishi yeyote wa serikali anayejiingiza katika kinyang’anyiro chochote cha kisiasa ndani ya siku 30 awe amejiuzulu nafasi yake.

Emefiele ameungana na Makamu wa Rais, Yemi Osibanjo, Gavana wa jimbo la Lagosi, Bola Tinubu na Waziri wa uchukuzi, Rotimi Amechi katika kuwania kuteuliwa kuwa mgombea urais wa chama hicho.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

KimataifaTangulizi

Mkuu wa majeshi Kenya afariki, Ruto atangaza maombolezo

Spread the loveRais wa Kenya, William Ruto ametangaza maombezo ya siku tatu...

Kimataifa

Majaji kuamua hatima ya Zuma leo

Spread the loveMajaji nchini Afrika Kusini leo Jumanne wataamua ikiwa rais wa...

Habari za SiasaKimataifa

Spika Afrika Kusini ajiuzulu kwa tuhuma za rushwa

Spread the loveSpika wa Bunge la Afrika Kusini, Nosiviwe Mapisa-Nqakula ametangaza kujiuzulu...

Habari MchanganyikoKimataifa

Tetemeko la ardhi laua 7, lajeruhi 800 Taiwan

Spread the loveWatu wapatao saba wamefariki dunia na wengine zaidi ya 800...

error: Content is protected !!