KUNDI la nchi saba zenye nguvu za kiviwanda duniani (G7), limejifungia nchini Japan kwa ajili ya kujadili vita kati ya Israel na Hamas, kundi la wanamgambo wa kiislamu linaloongoza ukanda wa Gaza, Palestina.Inaripoti Mitandao ya Kimataifa…(endelea).
Mawaziri wa mambo ya nje wa G7 inayojumusiha nchi za Canada, Ufaransa, Ujerumani, Italia, Japan na Marekani, pamoja na ujumbe wa Umoja wa Ulaya (EU),wamekutana katika kikao cha siku mbili kuanzia leo tarehe 7 hadi 8 Novemba 2023,Jijini Tokyo, nchini Japan.
Mkutano huo umeitishwa ikiwa vita hiyo imepigwa mfululizo wa siku 30, tangu Hamas wafanye shambulizi la kushtukiza upande wa Israel, Jumamosi ya tarehe 7 Oktoba mwaka huu, ambalo limepoteza maisha ya watu zaidi ya 1,400.
Kwa mujibu wa mitandao ya kimataifa, mkutano huo wa G7 umeitishwa baada ya idadi ya mauaji ya raia wasiokuwa na hatia kuongezeka, pamoja na hofu ya kwamba vita hiyo inaweza kuenea hadi kufikia kuwa janga la kikanda.
Hadi sasa, watu zaidi ya 10,000 wameripotiwa kufariki dunia upande wa Gaza.
Mbali na vita ya Israel na Hamas, pia G7 itajadili vita kati ya Urusi na Ukraine, mahusiano yake na China na namna ya kuimarisha mahusiano na nchi za Asia.
Leave a comment