Tuesday , 3 October 2023
Home Kitengo Habari Kimataifa Fedha za corona zamng’oa waziri
Kimataifa

Fedha za corona zamng’oa waziri

Ken Kandodo, Waziri wa Kazi wa Malawi
Spread the love

 

KEN Kandodo, Waziri wa Kazi wa Malawi na maofisa wengine wanne wa serikali ya nchi hiyo, wametimuliwa kazi kwa kukwapua fedha zilizotengwa kupambana na virusi vya corona (COVID-19). Inaripoti mitandao ya kimataifa … (endelea).

Maofisa hao wamefukuzwa kazi na Rais wa nchi hiyo, Lazarus Chakwera, baada ya kubaini ufisadi wa kwacha – fedha za Malawi – bilioni 6.2 (Dola za Marekani milioni 7.8) zilizotengwa kwa ajili ya kupambana na COVID-19.

Akitoa tamko la kuwafuta kazi maofisa hao, Rais Chakwera amesema, hakuna atakayesalimika na ukwapuaji wa fedha hizo huku akiarifu, tayari wahusika hao wapo kwenye vyombo vya sheria vya nchi hiyo.

Kiongozi huyo wa Malawi amesema, maofisa wengine waliohusika na ufisadi wa fedha hizo, watakamatwa katika siku zijazo huku akisisitiza, ripoti inaendelea kufanyiwa kazi.

“Siwezi kuwa na watu ndani ya baraza langu la mawaziri ambao wanatumia visivyo fedha zilizopangiwa kwa malengo tofauti,” amesema Rais Chakwera.

Waziri huyo ametuhumiwa kutumia vibaya kwacha 613,000 za Malawi zilizotengwa kwa ajili ya kupambana na corona.

Rais Chakwera amesema, licha ya waziri huyo kurejesha fedha, amesema hatua ya kutumia vibaya imejenga picha mbaya kwake na Taifa.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Kimataifa

Urusi yafungua milango kwa nchi za Afrika

Spread the loveSERIKALI ya Urusi imefungua milango ya ushirikiano wa kiuchumi, kijamii...

Kimataifa

Wadukuzi wa Kichana waiba barua pepe 60,000 za Serikali ya Marekani

Spread the loveWADUKUZI wa kichana wamedukua barua pepe 60000 serikali ya Marekani...

Kimataifa

Putin aita vikundi vya kujitolea vita ya Ukraine

Spread the loveRAIS wa Urusi, Vladimir Putin, amefungua milango ya ushirikiano kwa...

Kimataifa

Mlipuko wa bomu waua 50 katika sherehe za Maulidi ya Mtume

Spread the loveWATU takribani 50 wamefariki dunia huku wengine 50 wakijeruhiwa katika...

error: Content is protected !!