Friday , 26 April 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa Fedha za corona zamng’oa waziri
Kimataifa

Fedha za corona zamng’oa waziri

Ken Kandodo, Waziri wa Kazi wa Malawi
Spread the love

 

KEN Kandodo, Waziri wa Kazi wa Malawi na maofisa wengine wanne wa serikali ya nchi hiyo, wametimuliwa kazi kwa kukwapua fedha zilizotengwa kupambana na virusi vya corona (COVID-19). Inaripoti mitandao ya kimataifa … (endelea).

Maofisa hao wamefukuzwa kazi na Rais wa nchi hiyo, Lazarus Chakwera, baada ya kubaini ufisadi wa kwacha – fedha za Malawi – bilioni 6.2 (Dola za Marekani milioni 7.8) zilizotengwa kwa ajili ya kupambana na COVID-19.

Akitoa tamko la kuwafuta kazi maofisa hao, Rais Chakwera amesema, hakuna atakayesalimika na ukwapuaji wa fedha hizo huku akiarifu, tayari wahusika hao wapo kwenye vyombo vya sheria vya nchi hiyo.

Kiongozi huyo wa Malawi amesema, maofisa wengine waliohusika na ufisadi wa fedha hizo, watakamatwa katika siku zijazo huku akisisitiza, ripoti inaendelea kufanyiwa kazi.

“Siwezi kuwa na watu ndani ya baraza langu la mawaziri ambao wanatumia visivyo fedha zilizopangiwa kwa malengo tofauti,” amesema Rais Chakwera.

Waziri huyo ametuhumiwa kutumia vibaya kwacha 613,000 za Malawi zilizotengwa kwa ajili ya kupambana na corona.

Rais Chakwera amesema, licha ya waziri huyo kurejesha fedha, amesema hatua ya kutumia vibaya imejenga picha mbaya kwake na Taifa.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

KimataifaTangulizi

Mkuu wa majeshi Kenya afariki, Ruto atangaza maombolezo

Spread the loveRais wa Kenya, William Ruto ametangaza maombezo ya siku tatu...

Kimataifa

Majaji kuamua hatima ya Zuma leo

Spread the loveMajaji nchini Afrika Kusini leo Jumanne wataamua ikiwa rais wa...

Habari za SiasaKimataifa

Spika Afrika Kusini ajiuzulu kwa tuhuma za rushwa

Spread the loveSpika wa Bunge la Afrika Kusini, Nosiviwe Mapisa-Nqakula ametangaza kujiuzulu...

Habari MchanganyikoKimataifa

Tetemeko la ardhi laua 7, lajeruhi 800 Taiwan

Spread the loveWatu wapatao saba wamefariki dunia na wengine zaidi ya 800...

error: Content is protected !!