Monday , 5 June 2023
Home Habari Mchanganyiko Chalamila amkingia kifua Hayati Magufuli
Habari Mchanganyiko

Chalamila amkingia kifua Hayati Magufuli

Albert Chalamila, Mkuu wa Mkoa wa Mbeya
Spread the love

 

ALBERT Chalamila, Mkuu wa Mkoa wa Mbeya, amesema wanaojadili kwamba Hayati John Magufuli alikuwa dikteta, wanachosha akili. Anaripoti Mwandishi Wetu, Mbeya … (endelea).

Chalamila ametoa kauli hiyo leo tarehe 19 Aprili 2021, wakati akizungumza na wachimbaji wadogo wa madini katika Wilaya ya Chunya, mkoani humo.

Ametaka watu kutoingizwa kwenye mkumbo wa wale wanaosema, Hayati Magufuli aliyefariki dunia tarehe 17 Machi 2021, alikuwa dikteta katika utawala wake.

“Wengine nimesikia kwenye mijadala wanasema, Rais Magufuli alikuwa dikteta, ukimuona mtu anatokea sasa hivi anaanza kuongea wakati aliyekuwa Rais (Magufuli) amefariki, ujue huo ni mjadala hewa, msijiingize kwenye mijadala hiyo.”

“Ilifaa mumfikishie ujumbe wakati akiwa hai, mkianza kueleza mambo ambayo yeye amefariki, mnatuchosha akili,” amesema Chalamila akisitiza, mijadala inayoweza ‘kuwatoa kimaisha’ ni kuhusu kufanya kazi kwa bidii.

Chalamila amesema, watu hao walipaswa kumfikishia ujumbe Hayati Magufuli wakati akiwa hai kwamba yeye ni dikteta.

“Mijadala sahihi itakayotutoa kimaisha ni kazi, sio mijadala hewa…, mjadala wa kweli ni kuuliza umeme uko wapi? mbona barabara haijatengenezwa? mbona mawasiliano hakuna?

“Mjadala wa kweli nikusema hapa kuna watu wanatudai kodi wanatunyanganya kwa nguvu, tupate vituo vya afya vizuri, shule nzuri, tuwe na maisha bora. Mijadala hewa tuipotezee, haitatufikisha tunakokwenda,” amesema.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Tunduma watenga 60 milioni kujenga machinjio ya kisasa

Spread the loveHALMASHAURI ya mji Tunduma Imetenga kiasi cha Tshs Miloni 60...

Habari Mchanganyiko

Bilioni 17 kujenga bandari kavu Tunduma

Spread the loveHALMASHAURI ya mji Tunduma iliyopo wilayani  Momba mkoani Songwe imepatiwa...

Habari Mchanganyiko

Bandari ya Kigoma kuongezewa uwezo wa kutoa huduma zake

Spread the love  SERIKALI kupitia mamlaka ya Bandari nchini (TPA), imewekeza takribani...

Habari MchanganyikoTangulizi

Kifo cha mwanafunzi UDOM: Tume yamsafisha naibu waziri

Spread the loveTUME ya Haki za Binadamu na Utawala Bora nchini (THBUB),...

error: Content is protected !!