MCHEKASHAJI maarufu kutoka nchini Kenya Eric Omondi ametiwa mbaroni na jeshi la polisi nchini humo, kwa tuhuma za kuongoza kundi la vijana katika maandamano nje ya Bunge. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea)
Omondi ameongoza maandamano ya kundi la vijana kwa lengo la kupaza sauti wakiitaka serikali kuhakikisha inashusha gharama za maisha nchini humo.
Vijana hao walikuwa vifua wazi huku wakiwa wamevalia minyororo shingoni na kushikilia mabango yenye jumbe mbalimbali za kuonesha kutoris=dhishwa na ugumu wa maisha.
Kutokana na maandamano hayo, inaelezwa kuwa sehemu kubwa ya biashara katika eneo linalozunguka Bunge, zililazika kusitishwa kwa muda kutokana na hofu ya usalama.
Inadaiwa kuwa polisi wamelazimika kuingilia kati maandamano hayo na kuwaamuru waandamanaji hao kutawanyika, bila mafanikio, jambo lililowalazimu kuwatawanya kwa kutumia mabomu ya kutoa machozi na kumkamata kiongozi wa maandamano hayo mchekeshaji Omondi na baadhi ya waandamanaji.
Leave a comment