Wednesday , 29 March 2023
Home Kitengo Habari Kimataifa Eric Omondi mbaroni kwa kuongoza maandamano Kenya
Kimataifa

Eric Omondi mbaroni kwa kuongoza maandamano Kenya

Spread the love

 

MCHEKASHAJI maarufu kutoka nchini Kenya Eric Omondi ametiwa mbaroni na jeshi la polisi nchini humo, kwa tuhuma za kuongoza kundi la vijana katika maandamano nje ya Bunge. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea)

Omondi ameongoza maandamano ya kundi la vijana kwa lengo la kupaza sauti wakiitaka serikali kuhakikisha inashusha gharama za maisha nchini humo.

Vijana hao walikuwa vifua wazi huku wakiwa wamevalia minyororo shingoni na kushikilia mabango yenye jumbe mbalimbali za kuonesha kutoris=dhishwa na ugumu wa maisha.

Kutokana na maandamano hayo, inaelezwa kuwa sehemu kubwa ya biashara katika eneo linalozunguka Bunge, zililazika kusitishwa kwa muda kutokana na hofu ya usalama.

Inadaiwa kuwa polisi wamelazimika kuingilia kati maandamano hayo na kuwaamuru waandamanaji hao kutawanyika, bila mafanikio, jambo lililowalazimu kuwatawanya kwa kutumia mabomu ya kutoa machozi na kumkamata kiongozi wa maandamano hayo mchekeshaji Omondi na baadhi ya waandamanaji.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Kimataifa

Nyumba ya babu yake Makamu wa Rais wa Marekani yatafutwa Zambia

Spread the love  KAMALA Harris, makamu wa rais wa Marekani, amepanga kutembelea...

Kimataifa

Benki ya Uswizi mbioni kuziwekea vikwazo akaunti za siri za Wachina

Spread the love  WAKATI Serikali na Benki ya Uswizi ikichukua hatua kali...

Kimataifa

Netanyau asitisha mipango yenye utata marekebisho mfumo wa sheria

Spread the love  WAZIRI Mkuu wa nchini Israel, Benjamin Netanyahu amesema atachelewesha...

Kimataifa

Raila ahutubia waandamanaji, mabomu yarindima

Spread the loveMSAFARA wa kiongozi wa Azimio la Umoja-One Kenya, Raila Odinga...

error: Content is protected !!