Rais wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, Felix Tshisekedi amemteua waziri wa mipango, Judith Suminwa kuwa waziri mkuu wa nchi hiyo. Inaripoti Mitandao ya Kimataifa … (endelea).
Suminwa ni mwanamke wa kwanza kushika wadhifa huo wa waziri mkuu nchini Kongo. Uteuzi wa Suminwa unakamilisha wiki kadhaa zilizoghubikwa na hali ya sintofahamu kuhusu wadhifa huo.
Katika hotuba kupitia televisheni ya taifa, Suminwa amesema kuwa anafahamu kuhusu jukumu kubwa linalomkabili ni kufanya kazi kwa bidii pamoja na kuhakikisha kuwepo kwa amani na maendeleo nchini humo.
Kuapishwa kwa Tshisekedi kwa muhula wa pili madarakani mwezi Januari, kulianzisha mchakato wa muda mrefu wa kutafuta muungano wa vyama vingi katika bunge la kitaifa, ikiwa ni hatua muhimu kabla ya kuteuliwa kwa waziri mkuu na kuundwa kwa serikali.
Leave a comment