Wednesday , 1 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Dodoma kinara ukaguzi miradi mbio za mwenge 2023
Habari za Siasa

Dodoma kinara ukaguzi miradi mbio za mwenge 2023

Spread the love

MKOA wa Dodoma umeshika nafasi ya kwanza kati ya mikoa 31 kwa mwaka 2023 katika miradi iliyokaguliwa na kuzinduliwa na mbio za Mwenge nchini. Anaripoti Danson Kaijage, Dodoma… (endelea).

Hayo yamebainishwa na leo tarehe 29 Novemba 2023 na Mkuu wa Mkoa wa Dodoma,  Rosemary Senyamule katika kikao kazi kilichofanyika jijini humo na kujumuisha wakuu wa wilaya, wakurugenzi wa halmashauri na wataalam mbalimbali wa  ofisi ya mkuu wa mkoa.

Amesema mkoa huo umepanda kutoka nafasi ya 22 kati ya 31 kwa mwaka 2022 na kushika nafasi ya kwanza kati ya mikoa 31 kwa 2023.

Ni katika ukaguzi, uzinduzi wa miradi na shamrashamra za namna viongozi walivyoshiriki katika kukimbiza Mwenge wa Uhuru mkoani Dodoma.

“Tumetumia siku ya leo kufanya tathmini kama ambavyo huwa tunafanya miaka yote ya kuona namna ambavyo tumetekeleza ubora wa miradi na vigezo vingine vilivyowekwa katika shughuli za Mwenge wa Uhuru.

“Tunamshukuru Mungu halmashauri tano za Dodoma Jiji, Kondoa DC na TC, Mpwapwa na Kongwa zimeingia katika 10 bora ya Taifa.

“Mwaka jana 2022 mkoa ulishika nafasi ya 22 hatukupendezwa na matokeo hayo, tulipeana shime ya kuifaharisha Dodoma na tukaungana kupambania mkoa na tunamshukuru Mungu kwa mara ya kwanza tumeshika nafasi ya kwanza kitaifa tumeifahalisha Dodoma na makao makuu ya nchi,” amebainisha Senyamule.

Katika kuelekea msimu wa kilimo Afisa kilimo wa Mkoa wa Dodoma, Bernald Abraham amesema wapo tayari kwa uzinduzi wa msimu wa kilimo unaotarajiwa kuzinduliwa Novemba 29 mwaka huu katika kata ya mazae wilayani Mpwapwa.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mavunde ataja malengo “Vision 2030”

Spread the loveWAZIRI wa Madini amesema dhana ya “Vision 2030” inakusudia kuiendeleza...

Habari za Siasa

Mavunde aomba bilioni 231.9 bajeti wizara ya madini

Spread the loveWAZIRI wa Madini, Anthony Mavunde leo Jumanne amewasilisha hotuba ya...

Habari za SiasaTangulizi

Lissu amjibu Fatma Karume kuhusu Rais Samia

Spread the love  MAKAMU Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema)...

Habari za SiasaTangulizi

Dk. Slaa: Watanzania iungeni mkono Chadema uchaguzi 2025

Spread the loveMWANASIASA mkongwe nchini Tanzania, Dk. Wilbroad Slaa, amewataka watanzania wakiunge...

error: Content is protected !!