Wednesday , 1 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa RC Dodoma: Kila kaya, taasisi zilime heka 2 mazao ya chakula
Habari za Siasa

RC Dodoma: Kila kaya, taasisi zilime heka 2 mazao ya chakula

Spread the love

KATIKA harakati za kuimarisha sekta ya kilimo pamoja na kuhamasisha  wananchi kulima mazao yenye tija ili kuondokana na baa la njaa, Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Rosemary Senyamule ameagiza kila kaya na taasisi ikiwamo shule zilime heka mbili za mtama pamoja na mazao mengine ya chakula katika msimu wa kilimo 2023/2024.

Ametaja mazao hayo yanayopewa kipaumbele kuwa mbali na mtama, ni uwele, mpunga, mhogo, viazi vitamu, maharage, kunde, mbaazi, njegere, choroko, viazi mviringo na mahindi. Anaripoti Danson Kaijage, Mpwapwa (endelea).

Senyamule ametoa maagizo hayo leo tarehe 29 Novemba 2023 katika hafla ya uzinduzi wa msimu wa kilimo 2023 /2024.

Uzinduzi huo umehusisha wataalamu, maafisa kilimo kwa lengo la  kusaidia wakulima kulima kilimo cha uhakika wa chakula, afya bora, ajira na kukuza uchumi kwa mtu mmmoja mmoja na Serikali.

Uzinduzi huo umefanyika leo tarehe 29 Novemba 2023 katika viwanja vya Shule ya Sekondari Mazae Wilayani Mpwapwa Mkoani Dodoma.

Amesema malengo ya msimu wa kilimo 2023/2024 ni kila kaya na taasisi kama shule lazima kulima angalau heka mbili za mtama.

Ameongeza kuwa matarajio ni kulima tani 170,235 za mazao ya biashara ni alizeti, korosho, karanga na ufuta tani 13,350.

Aidha, Senyamule ametoa wito kwa maafisa Kilimo kufanya hamasa ya kutosha kijiji kwa kijiji kwa kulima kufanya shughuli za kilimo, kufanya kazi ya kuwapimia udongo wananchi ili kuwasaidia kujua aina ya mazao ya kulima kwenye mazingira yao pamoja na kutoa elimu kwa wananchi kuhusu umuhimu wa mbegu bora na kuwaunganisha na taasisi za kilimo.

Kwa upande wake, Katibu Tawala Mkoa wa Dodoma, Ally Gugu ametoa wito kwa wakulima wote wa mkoa huo na Taifa kwa ujumla kuzingatia elimu wanayopewa na wataalamu wa kilimo ili kuongeza uzalishaji.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mavunde ataja malengo “Vision 2030”

Spread the loveWAZIRI wa Madini amesema dhana ya “Vision 2030” inakusudia kuiendeleza...

Habari za Siasa

Mavunde aomba bilioni 231.9 bajeti wizara ya madini

Spread the loveWAZIRI wa Madini, Anthony Mavunde leo Jumanne amewasilisha hotuba ya...

Habari za SiasaTangulizi

Lissu amjibu Fatma Karume kuhusu Rais Samia

Spread the love  MAKAMU Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema)...

Habari za SiasaTangulizi

Dk. Slaa: Watanzania iungeni mkono Chadema uchaguzi 2025

Spread the loveMWANASIASA mkongwe nchini Tanzania, Dk. Wilbroad Slaa, amewataka watanzania wakiunge...

error: Content is protected !!