KATIBU Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Balozi Emmanuel Nchimbi, amesema Rais Samia ana dhamira ya dhati katika kuimarisha na kuboresha uhusiano wa nchi na vyama rafiki katika ukombozi wa Mataifa ya Kusini Kwa Afrika. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam…(endelea).
Balozi Nchimbi aliyasema hayo jana Jumanne, katika Mkutano wa 11 wa makatibu wakuu wa vyama vya rafiki vya ukombozi wa Kusini mwa Afrika, unaoendelea nchini Zimbabwe.
Katika hatua nyingine, Balozi Nchimbi alisema CCM inajivunia juu ya uongozi wa Rais Samia aliyetimiza miaka mitatu madarakani tarehe 19 Machi mwaka huu, kufuatia kifo cha mtangulizi wake Hayati John Magufuli, kilichotokea tarehe 17 Machi 2021.
“Kwa kweli ninajivunia sana Rais Samia si Kwa sababu tu Mimi ni mpigania haki za Wanawake, bali kwa sababu ya uwezo wake mkubwa wa uongozi mzuri anavyoendelea kuingiza nchi yetu. Kutokana na hilo CCM inajivunia uongozi wake na wananchi wote kwa ujumla tunajivunia kuongozwa na Rais Samia Kwa uwezo wake aliouonesha Kwa miaka mitatu hii,” alisema Balozi Nchimbi.
Leave a comment