MAKAMU Rais Dk. Philip Mpango leo tarehe 5 Septemba, 2022, amewasili Kigali nchini Rwanda Kumwakilisha Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan katika mkutano wa Mapinduzi ya Kijani Barani Afrika mwaka 2022. Anaripoti Juliana Assenga, UDSM … (endelea).
Mkutano huo wa wapinduzi ya kijani Barani Afrika (AGRF 2022) unatarajiwa kufanyika kesho tarehe 6 septemba 2022 ukiwa na lengo mahususi la kujadili hatua madhubuti kwa ajili ya mifumo ya chakula inayostahimili.
Mkutano huo pia utashirikisha wakuu wa Nchi na serikali kutoka mataifa mbalimbali ya Afrika, viongozi wa Taasisi na Jumuiya za kimataifa pamoja na wadau wote wa kilimo.
Leave a comment